Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/07 uku. 1
  • ‘Sema Neno la Mungu Bila Woga’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Sema Neno la Mungu Bila Woga’
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Mwige Yesu—Hubiri Kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Julisha Rasmi Habari Njema kwa Ujasiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Je, Wahubiri kwa Ujasiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 4/07 uku. 1

‘Sema Neno la Mungu Bila Woga’

1 Je, nyakati nyingine wewe unasita kuzungumza kuhusu mambo unayoamini unapopata nafasi ya kufanya hivyo shuleni au kazini? Je, ni vigumu kuwahubiria isivyo rasmi watu wa ukoo, majirani, au watu usiowajua? Ni nini kitakachotusaidia sisi sote kutumia nafasi zinazofaa “kulisema neno la Mungu bila woga”?—Flp. 1:14.

2 Usisite: Je, ungesita kumtetea rafiki yako wa karibu au mtu wa ukoo ambaye anashtakiwa kwa uwongo? Yehova, Rafiki yetu wa karibu, ameshtakiwa isivyo kweli kwa maelfu ya miaka. Tuna pendeleo la pekee la kutoa ushahidi kwa ajili ya Mungu wetu mkuu! (Isa. 43:10-12) Kumpenda Yehova sana kunaweza kutusaidia kukabiliana na hisia za woga na kutuchochea kusema, tukitoa ushahidi kuhusu kweli kwa ujasiri na bila kujizuia.—Mdo. 4:26, 29, 31.

3 Kumbuka kwamba unahubiri kuhusu habari njema. Kutii habari hizo kutawapa watu manufaa ya kudumu. Tutahubiri kwa ujasiri ikiwa tutakazia fikira thamani ya kazi ya kuhubiri badala ya kujikazia fikira au kuwakazia fikira wale wanaotupinga.

4 Mifano ya Wengine: Tunaweza kupata nguvu kutokana na uaminifu wa wengine ambao wamesema neno la Mungu bila woga. Kwa mfano, Enoko alitangaza kwa ujasiri hukumu ya Yehova dhidi ya watenda dhambi wasiomwogopa Mungu. (Yuda 14, 15) Noa aliwahubiria kwa uaminifu watu ambao hawakujali. (Mt. 24:37-39) Wakristo wa karne ya kwanza ambao walikuwa watu “wasio na elimu na wa kawaida tu” waliendelea kuhubiri licha ya upinzani mkali. (Mdo. 4:13, 18-20) Mara nyingi Mnara wa Mlinzi na Amkeni! huwa na masimulizi ya wakati wetu kuhusu maisha ya wale ambao kwa sababu ya kuwa na imani katika Yehova waliacha kuwaogopa wanadamu na kuwa wahubiri wenye bidii.

5 Tunaweza kupata ujasiri kwa kufikiria maisha ya watumishi waaminifu wa kale ambao walikabiliana na hali ngumu. (1 Fal. 19:2, 3; Marko 14:66-71) ‘Walijipa ujasiri kwa njia ya Mungu wetu’ na hivyo wakasema bila woga. Sisi pia tunaweza kufanya hivyo!—1 The. 2:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki