Julisha Rasmi Habari Njema kwa Ujasiri
1 Kihistoria, Wakristo wa kweli wanajulikana kwa ajili ya ujasiri wao. Mitume Petro na Yohana ni vielelezo vya kutokeza vya jambo hilo. Wajapotupwa ndani ya gereza na kutishwa, mitume hao waliendelea bila hofu na kwa ujasiri kunena ukweli. (Matendo 4:18-20, 23, 31b) Pia Paulo aliendelea kwa ujasiri na huduma yake katika eneo gumu hata ijapokuwa alipatwa na mateso mengi.—Matendo 20:20; 2 Kor. 11:23, 28.
2 Ikoje kwamba ijapokuwa uhasama mkubwa, mitume na pia Wakristo wengine katika historia yote waliweza kuendelea kujulisha rasmi habari njema kwa ujasiri? Mtume Paulo anajibu swali hilo kwenye 1 Wathesalonike 2:2, ambapo anasema, “Twalithubutu katika Mungu kuinena Injili [habari njema, NW] ya Mungu kwenu.” Hali moja na hiyo, Petro na Yohana na pia wanafunzi wengine waliweza kupiga mbiu ya habari njema kwa ujasiri. Baada ya kufunguliwa kutoka pingu zao za gereza, Petro na Yohana waliripoti kwa wanafunzi wenzao. Katika sala walimsihi Yehova awape moyo mkuu na nguvu ‘za kuendelea kunena neno lake kwa ujasiri wote.’ Sala hiyo ilijibiwa mara na Mungu wakati “wao mmoja kwa wote walipojazwa kwa roho takatifu na walikuwa wakinena neno la Mungu kwa ujasiri.”—Mdo. 4:29, 31, NW.
KUONYESHA ITIBARI KATIKA YEHOVA
3 Mitume walikuwa na itibari Yehova alikuwa akiwategemeza. Ahadi zote ambazo Yehova alikuwa amefanya kupitia Neno lake zilikuwa zinathibitika kuwa kweli. Na zile zilizongoja kutimizwa zilikuwa zimehakikishwa kupitia Yesu Kristo. Je! sisi tuna itibari iyo hiyo ya kujulisha rasmi habari njema kwa ujasiri? Ingawa sisi hatuneni katika lugha wala kuponya wagonjwa, tungali tuna ushuhuda tele wa kuungwa mkono na Yehova. Tunapoona utimizo wa unabii wa Biblia, je! sisi tunachochewa tunene habari njema za Ufalme wa Mungu kwa ujasiri?
4 Hata hivyo, ni jambo la kutazamiwa kwamba kuhubiri kwa ujasiri hivyo kutakabiliana na upinzani. (Yn. 15:20) Ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu na Wakristo wa karne ya kwanza. Lakini hilo halikuwazuia wala kupunguza bidii ambayo walihubiri nayo. Kwa kweli, upinzani huo mara nyingi uliwapa fursa kubwa zaidi za kueneza habari njema za Ufalme. (Mdo. 4:3, 8-13a) Kwa sababu ya kuambatana kwetu kwa Kikristo na Neno la Mungu juu ya masuala ya muhimu, nyakati nyingi sisi tunatakwa tutoe sababu kwa ajili ya msimamo wetu. Sisi huona pindi hizo kuwa fursa za kujulisha rasmi habari njema kwa ujasiri. Kwa kufanya hivyo, sisi tunamwiga Yesu Kristo na mitume wake.
5 Kufanya upainia msaidizi kunatupa fursa kubwa zaidi za kujulisha rasmi habari njema. Wengi watakuwa wakifanya upainia msaidizi wakati wa Aprili na Mei, hali wengine wanapanga kufanya hivyo wakati wa miezi inayokuja. Je! mastakimu zako zitakuruhusu utoe ombi? Kwa kufanya jitihada ya kushiriki katika kazi ya upainia msaidizi, tunajithibitisha wenyewe kuwa kama Paulo na Barnaba. Kwenye Matendo 14:3 husema kwamba ‘walikaa wakati mwingi, wakinena kwa ushujaa [kwa ujasiri, NW] katika Bwana [Yehova, NW].’ Kama tunaweza kununua wakati kutoka utendaji mwingine tutumie angalau saa 60 katika huduma ya shambani wakati wa mwezi mmoja, baraka zetu bila shaka zitaongezeka.
6 Kuwa wajasiri katika huduma ni msaada hasa wakati wa kutoa maandikisho. Magazeti hayo yana ujumbe wa kuokoa uhai unaotegemea Neno la Mungu. Kwa hiyo tusisite bali tuhubiri kwa ujasiri kwa kuiga Kielelezo chetu, Yesu, na mitume wake.