Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/90 uku. 2
  • Mikutano Inayosaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayosaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA APRILI 2
  • JUMA LINALOANZA APRILI 9
  • JUMA LINALOANZA APRILI 16
  • JUMA LINALOANZA APRILI 23
  • JUMA LINALOANZA APRILI 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 4/90 uku. 2

Mikutano Inayosaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA APRILI 2

Wimbo 87

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote kwamba Ukumbusho utakuwa Jumanne jioni, Aprili 10. Taja saa za sherehe, na ueleze kifupi mipango ya mahali penu. Jitihada ya pekee ifanywe kwenye mwisho-juma ili kualika watu wanaopendezwa. Toa wonyesho wa kualika mwanafunzi wa Biblia kwenye Ukumbusho.

Dak. 20: “Dini Inayompendeza Mungu.” Zungumza Kichwa cha Mazungumzo kipya pamoja na wasikilizaji. Mhubiri mwenye uwezo atoe wonyesho wa mahubiri yafuatayo yaliyopendekezwa: “Watu wengi leo wana wasiwasi na wamevurugika kuona dini nyingi sana zenye kupingana. Ndivyo na wewe, sivyo? Wengine wamesema kwamba dini mbalimbali ni barabara tu zinazoongoza mahali pale pamoja pa wokovu. Je! hayo ndiyo maoni aliyokuwa nayo Yesu Kristo? Angalia maneno yake kwenye Mathayo 7:13, 14: (Soma) Kwa hiyo Yesu hakufundisha kwamba dini zote zinakubalika kwa Mungu. Basi tunaweza kuhakikishaje tuko kwenye njia nyembamba inayoongoza kwenye wokovu na tunamwabudu Mungu katika njia inayokubalika Kwake? Biblia inaonyesha hapa kwenye Efeso 4:5, 13 kwamba takwa moja ni umoja kati ya waabudu. (Soma.) Kwa wazi, kwapasa kuwe amani wala si migawanyiko wala vita kati ya wale walio na dini inayompendeza Mungu. Angalia pia katika mstari wa 13 umaana wa kuwa na maarifa sahihi ya Mwana wa Mungu. Hilo linataka kupata kujua ambayo Biblia inafundisha juu ya Yesu na uhusiano wake pamoja na Mungu. Ndiyo sababu tunatia moyo funzo la Biblia. Takwa moja la mwisho ambalo tungependa kutaja wakati huu ni kwamba, ili kuwa na dini inayompendeza Mungu ni lazima mtu aishi kulingana na viwango vya adili vya juu vya Biblia kama inavyoonyeshwa kwenye Tito 1:16 (Soma. Toa kielelezo kimoja au viwili kama vile uhaki au adili za kingono.) Habari zaidi juu ya jinsi ya kuabudu katika njia inayompendeza Mungu zaweza kupatikana katika gazeti Mnara wa Mlinzi. Kwa kielelezo (rejezea jambo fulani hususa katika toleo (matoleo) la karibuni.

Dak. 15: “Ukumbusho—Sherehe ya Kikristo.” Maswali na majibu. Baada ya fungu 6, kwa ufupi toa wonyesho wa ziara ya kukumbusha mtu aliyekuwa ametangulia kualikwa, halafu uulize kundi lisimulie jinsi wanavyopanga kuwaalika wapya kwenye Ukumbusho na kuwasaidia wahudhurie. Kumbusha kundi kwamba mialiko iliyochapishwa inapatikana.

Wimbo 181 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 9

Wimbo 148

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Toa wonyesho wa mahubiri mawili ya sekunde 30 hadi 60 ya kutoa magazeti ya karibuni. Julisha kundi juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Machi. Wasifu kwa ajili ya kazi nzuri iliyotimizwa.

Dak. 15: “Heshimu Yesu Kristo—Msingi wa Imani Yetu.” Mazungumzo ya maswali na majibu.

Dak. 17: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutoa Maandikisho kwa Ujasiri.” Maswali na majibu. Baada ya fungu 4, toa wonyesho wa kutumia Kichwa cha Mazungumzo kipya. Anayetoa mahubiri apaswa kuwa chanya wakati wa kutoa andikisho.

Wimbo 193 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 16

Wimbo 23

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayohusu katika Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 20: “Julisha Rasmi Habari Njema kwa Ujasiri.” Mazungumzo ya habari kwa maswali na majibu. Mafungu yasomwe kwa kadiri wakati unavyoruhusu.

Dak. 15: Maoni ya Biblia. Hotuba na wonyesho. Tangu toleo la Amkeni! la Februari 8, 1987, “Maoni ya Biblia” imekuwa sehemu ya kupendeza ya gazeti hilo. Makala hizo kuhusu msimamo wa Biblia juu ya habari zilizozungumzwa zimekusudiwa kwa ajili ya akili yenye utafiti, mtu aiamini asiiamini Biblia. Mara nyingi makala hizo zinatoa mfikio mpya kwa habari zilizokwisha kuelezwa hapo awali. Je! tunatumia sehemu hii katika huduma ya shambani? Makala hizo ni fupi na zinaipiga shabaha yenyewe, zikiwa na urefu wa kurasa mbili. Pitia pamoja na wasikilizaji baadhi ya makala hizo zinazofaa eneo la mahali penu. Toa wonyesho jinsi makala hizo zaweza kutumiwa katika huduma.

Wimbo 92 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 23

Wimbo 106

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Mnenaji apaswa pia kuzungumza na wasikilizaji yanayoweza kusemwa wakati wa kutumia toleo la karibuni la Mnara wa Mlinzi.

Dak. 25: “Hekimika—Tumia Mambo Unayojifunza.” Mzee azungumza habari na wasikilizaji. Kazia uhitaji wa kujifunza vichapo kwa uangalifu ili yale yanayojifunzwa yaweze kukumbukwa na kutumiwa. Elekeza fikira kwenye mambo fulani yanayohusu katika vichapo vya karibuni ambayo yanatumika mahali penu. Vielelezo: jinsi vijana wanavyoweza kushughulika na hali shuleni; jinsi ya kushughulikia matatizo yanayokabiliwa mahali pa kazi, jinsi ya kutatua matatizo baina ya ndugu au wenzi wa ndoa. Tumia habari itakayosaidia zaidi kundi la mahali penu.

Dak. 10: Baraka Zinazotokana na Kutumia Yale Tunayojifunza. Mambo yaliyoonwa yaliyotayarishwa vizuri yasimuliwe juu ya jinsi mambo yaliyojifunzwa yametumiwa na baraka ambazo watu mmoja mmoja walioyatumia wamepata. Mambo yaliyoonwa ya mahali penu yafaa zaidi, lakini ikihitajiwa, yale katika 1990 Yearbook yaweza kutumiwa.—Ona kurasa 7-9, 43-5, 50-3, 57-8, 64.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 30

Wimbo 200

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja hesabu ya maandikisho mapya yaliyopatikana na kundi, na uulize mambo yaliyoonwa ambayo yalionewa shangwe na wale ambao wanafanya upainia msaidizi wakati wa mwezi.

Dak. 20: “Kutayarisha kwa Ajili ya Mafunzo ya Biblia.” Mazungumzo ya kupitia Maandiko yote na mambo yenye kuunga mkono makala hiyo yenye kichwa hicho katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1989.

Dak. 15: Thamani ya Habari Njema Maishani Mwetu. Hotuba. Habari yaweza kupatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1990, kurasa 4-6. Panga maelezo yaliyotayarishwa kutoka kundi juu ya jinsi habari njema zimewasaidia wafanye maisha zao kuwa bora zaidi.

Wimbo 72 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki