Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 1/1 kur. 4-6
  • Utangazaji wa Habari Njema Duniani Pote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utangazaji wa Habari Njema Duniani Pote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sasa Hafanyi Bima ya Maisha
  • Fungu la Thamani za Kiadili Zilizobadilika
  • Ndoa Iliyorekebishwa Ikawa Sawa
  • Maisha Yaliyobadilika
  • Habari Njema Gerezani
  • Habari Njema kwa Aina ya Binadamu Yote!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • ‘Habari Njema Zenye Utukufu Kutoka kwa Mungu Aliye na Furaha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Gospeli Yaweza Kukunufaishaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Njema kwa Wanadamu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 1/1 kur. 4-6

Utangazaji wa Habari Njema Duniani Pote

UFALME wa Mungu watawala! Hizi ndizo habari njema zilizo bora kupita zote. Ndiyo sababu katika 1989 Mashahidi wa Yehova zaidi ya 3,700,000 kuzunguka ulimwengu walipiga kwa idili mbiu ya “habari njema” zilizotabiriwa na Yesu na “taarifa teremeshi” zilizojulishwa wazi na malaika katika njozi ya Yohana. (Mathayo 24:14; Ufunuo 14:6, NW) Kama alivyosema mtume Paulo: ‘Sauti yao ilienea duniani mwote, na maneno yao hata miisho ya ulimwengu.’ (Warumi 10:18) Na kwa mteremo watu mmoja mmoja wa tuseme kila taifa na kabila na ulimi na kikundi waliitikia wito wao ‘kuhofu Mungu na kumpa yeye utukufu.’​—Ufunuo 14:7, NW.

Sasa Hafanyi Bima ya Maisha

Mtu mmoja wa jinsi hiyo alikuwa mwanamume mmoja katika Uingereza ambaye alijipatia riziki kwa kutegemea mashaka-mashaka ya maisha. Ken alikuwa muuzaji wa bima, na alipotembelea nyumba moja ya Mashahidi wa Yehova, wao walimuuliza hivi: “Wewe ungependa kuishi katika ulimwengu ambamo bima ya maisha haingehitajiwa kabisa?” Walimaanisha nini? Kwamba kulingana na Biblia, chini ya Ufalme wa Mungu mambo mengi ambayo yafanya maisha sasa yawe ya mashaka-mashaka sana, kutia na magonjwa na kifo, hayatakuwapo tena.

Je! jambo hilo lawezekana? Ndiyo, Mungu mwenyewe ameliahidi. Kwa kielelezo, Biblia yasema hivi: “Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao [aina ya binadamu]. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” (Ufunuo 21:3, 4) Ni jambo gani litakaloleta badiliko hilo? Ni Ufalme wa Mungu. Kulingana na Neno la Mungu, karibuni huo “utavunja falme hizi zote [za siasa za ki-siku-hizi] vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”​—Danieli 2:44.

Uangalifu wa mamia ya mamilioni ya watu ulielekezwa na Mashahidi wa Yehova kwenye maandiko kama haya wakati wa kampeni yao ya kuhubiri duniani pote. Watu wengi, kama Ken, walikuja kung’amua kwamba hii si fikira ya kuwazia-wazia tu mambo yasiyowezekana. Ushuhuda uliopo ni hakika kabisa. Ahadi hizi za kimungu ni za kutumainika na karibuni zitatimizwa.

Fungu la Thamani za Kiadili Zilizobadilika

Wale ambao husikiliza Mashahidi wa Yehova watoapo mwangwi wa ile mbiu yenye shangwe ya malaika huja kung’amua kwamba kuhofu Mungu na kumpa yeye utukufu kwahusisha ndani mambo mengi kuliko kuamini ahadi za Biblia tu. Hubadili tazamio lao zima na kupunguza uzito wa vitatanishi vingi vya maisha.

Rafael na mke wake walipata jambo hili kuwa kweli. Wao huishi katika Argentina, na walipofunga ndoa miaka zaidi ya 40 iliyopita, walifanya mradi wao mkubwa maishani uwe kufanya kazi kwa bidii na kuweka akiba ili wawe na wakati ujao salama. Hata hivyo, miaka 21 baadaye hawakuwa na kitu cha kuonyesha kutokana na kazi yao ya bidii isipokuwa nyumba ndogo iliyohitaji kutengenezwa daima. Hawakuhisi wakiwa salama zaidi ya wakati walipofunga ndoa mara ya kwanza.

Ndipo waliposikia habari njema kutoka kwa Mashahidi wa Yehova na wakajifunza juu ya utajiri wa aina bora na usalama wa aina bora zaidi. Yesu, katika Mahubiri ya Mlimani aliyoyatoa yeye, alinena juu ya jambo hili aliposema hivi: “Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi.”​—Mathayo 6:19, 20.

Ingawa Biblia haitufundishi tuwe na maoni yasiyofaa kuhusu utajiri wa kimwili, hiyo hutuhimiza tusitie tumaini letu katika vitu hivyo. (Mhubiri 7:12) Badala ya hivyo, yatupasa tufanye kazi kupata mali za kiroho kwa kujifunza Biblia, kujua penzi la Mungu ni nini, na kufanya utendaji wa penzi hilo uwe ndilo jambo la kwanza katika maisha zetu. (Mathayo 6:33) Rafael na mke wake walianza kurundika utajiri huu wa kiroho, na sasa wao wahisi wakiwa matajiri kikweli, si kwa sababu ya hali yao ya kifedha, bali kwa sababu ya uhusiano wao pamoja na Mungu. (Ufunuo 3:17, 18) Ujumbe wa Ufalme wa Mungu ulikuwa habari njema sana kwao.

Ndoa Iliyorekebishwa Ikawa Sawa

Habari njema zina nguvu halisi za kutimiza mema. Kwa kielelezo, John, ambaye huishi Uingereza, hakupendezwa na Biblia, lakini mke wake na watoto walipendezwa. Kwa hiyo walianza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova huku John akienda kunywa pamoja na rafiki zake. Tokeo ni kwamba, yeye alihusika katika unywaji wa kupindukia, kuvuta sigareti, na, hatimaye, katika ukosefu wa adili. Mwishowe, aliacha mke wake ili akaishi na mwanamke mwingine.

Hatua za talaka zilianza. Lakini John akashangaa kuona kwamba mke wake​—aliyekuwa amejifunza mwenendo wa Kikristo kutokana na funzo lake la habari njema​—bado alimtendea yeye kwa ufikirio. John hakuweza kuelewa sababu. Majuma matatu kabla shauri halijakatwa kabisa kuhusu talaka, mwenendo wa Kikristo wa mke wa John ulileta matokeo. Mwanamume huyo alionyesha masikitiko ya kweli kwa mwenendo wake, na hatua za talaka zikakomeshwa. Sasa John alizichunguza habari njema yeye mwenyewe na kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Sasa yeye pia ni Mkristo, na akiwa pamoja na mke wake, anawaambia wengine kuhusu habari njema za Ufalme.

Katika siku hizi za kubomoka-bomoka kwa thamani za kijamaa, watu wengi wahitaji msaada wenye kutolewa na habari njema zenye msingi wa Biblia. Mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika Peru alikuwa ameketi karibu na kanali wa jeshi wakati wa safari moja ya kuruka kwa ndege. Waliingilia maongeo fulani na kanali yule akaanza kumimina matata yake ya kijamaa, kutia na uhakika wa kwamba mke wake alikuwa mzoelevu wa dawa za kulevya na alikuwa karibu kumwacha ili akakae na mwanamume aliye kijana zaidi. Shahidi huyo akamwonyesha kwa busara kwamba Biblia hutoa ushauri mwema na ulio thabiti kuhusu mambo ya jamaa na kwamba ilimsaidia yeye binafsi atatue matatizo yake mwenyewe ya jamaa.​—Waefeso 5:21-6:4.

Kanali yule alimshukuru Shahidi kwa maneno yake yenye kufariji na akaandikisha awe akipata magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ili aweze kuendeleza maarifa yake juu ya habari njema. Ndipo, wakati Shahidi yule alipokuwa akiondoka kwenye ndege ile, mume na mke vijana wakafanya haraka kumfikilia na kuomba kwamba waongee naye. “Sisi tulikuwa tumeketi pale pale mbele yako,” wakasema, “nasi tukasikia maongeo yako na bwana yule. Sisi pia tungependa kuandikisha tuwe tukipata magazeti hayo.” Wao pia walitaka kujua juu ya habari njema ambazo zaweza kuleta nafuu katika maisha za watu.

Maisha Yaliyobadilika

Zaidi ya hilo, habari njema zenye msingi wa Biblia hubadili watu. Kama vile mtume Paulo alivyosema: “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu.” (Waebrania 4:12) Ndivyo ilivyokuwa katika kisa cha mwanamume kijana katika Makedonia, Ugiriki. Yeye aligutuka kujua kwamba, kulingana na Biblia, jina la Mungu ni Yehova. Kwa hiyo akaomba rafiki amkutanishe na Mashahidi wa Yehova mara iwezekanapo. Mazungumzo mawili yalipangwa pamoja na Mashahidi, kila moja likiwa la urefu wa karibu saa nne. Ndipo huyo mwanamume kijana akaanza funzo la Biblia la ukawaida, lile la kwanza likiendelea hadi saa nane ya usiku!

Kuanzia funzo hilo la kwanza, mwanamume kijana huyo alipatanisha maisha yake na viwango vya Biblia kwa haraka sana. Alihudhuria mikutano ili kuabudu pamoja na Mashahidi wa Yehova na akaja kumpenda sana Muumba. Naye Yehova akambariki. Juma la kwanza la funzo lake la Biblia, alikata nywele zake ndefu. Juma la pili, aliacha kwenda kwenye mikahawa na madisko (dansi) kutafuta waandamani wenye kusisimua. Juma la tatu, alitupilia mbali sigareti yake ya mwisho. Baada ya kujifunza kwa miezi miwili, alianza kujiunga na Mashahidi katika kuambia wengine habari njema za Ufalme. Ndiyo, aliterema kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wameleta habari njema kwenye sehemu yake ya dunia.

Habari Njema Gerezani

Hata mapingo ya gereza hayazuii habari njema. Katika Hispania mwanamume kijana ambaye jina lake ni Jose anatumika kifungo kirefu gerezani kwa sababu ya unyang’anyi wa kutumia silaha na vitendo vingine vya uhalifu. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova waliweza kumwambia habari njema, na ujumbe wa Biblia ukabadili kabisa matazamio yake. Yehova ‘alimtia nguvu.’​—Wafilipi 4:13.

Jose asema aweza kutumia maisha yake yaliyobaki katika mfumo huu wa mambo akiwa nyuma ya mapingo ya gereza kwa sababu ya mwenendo wake wa zamani. Lakini yeye amebatizwa na sasa ni Mkristo. Mke wake humuunga mkono kwa imara, na anajaribu kumpa mwana wao mchanga malezi ya Kikristo. Kwa wakati huu, Jose hushiriki habari njema pamoja na wafungwa wenzake, watu ambao ni vigumu kufikiwa na wale wenye kuishi nje ya kuta za gereza. Sasa mwenzake katika seli ni Mkristo aliyebatizwa pia.

Hivi ni vielelezo vichache tu vya kuonyesha matokeo ya kampeni ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri duniani pote. Kwa kweli, habari njema zilizojulishwa wazi na malaika yule asiyeonekana zimefanyiwa mwangwi na Mashahidi wa Yehova “kuwa taarifa teremeshi kwa wale ambao hukaa juu ya dunia, na kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu.”

Ndizo habari bora kuliko zote, nazo ndilo tumaini la pekee kwa aina ya binadamu. Twakuhimiza wewe uzitii. Kama vile Ken na John katika Uingereza, kama vile Rafael na mke wake katika Argentina, kama vile Jose katika Hispania, na kama vile mamiriadi ya wengine, sisi twajiunga na yule malaika katika kuhimiza wote ‘wamhofu Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili, na hivyo wamwabudu yule Mmoja ambaye alifanyiza mbingu na dunia na bahari na vibubujiko vya maji.’​—Ufunuo 14:7, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki