Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 12/15 kur. 5-7
  • Gospeli Yaweza Kukunufaishaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Gospeli Yaweza Kukunufaishaje?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Watu Waliosaidiwa na Gospeli
  • Habari Njema Humaanisha Nini Leo?
  • Nguvu ya Gospeli Leo
  • Baraka Zilizoko Mbele Bado
  • ‘Habari Njema Zenye Utukufu Kutoka kwa Mungu Aliye na Furaha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • ‘Kuleta Habari Njema za Jambo Bora’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Gospeli Kwa Kweli Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • “Habari Njema”!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 12/15 kur. 5-7

Gospeli Yaweza Kukunufaishaje?

BIBLIA huheshimiwa sana kwa ajili ya thamani yayo ya kielimu—hata na baadhi ya wale wasioamini kuwako kwa Mungu. Hata hivyo, kwa kweli, ni wachache wanaoisoma ili kutumia yale inayosema. Isitoshe, kwa kuwa habari njema zilizomo katika Biblia zina tarehe ya tangu karibu miaka elfu mbili iliyopita, yaonekana watu wengi huamini kwamba inapaswa kufanywa kuwa ya ki-siku-hizi, kufanywa upya. Je! Gospeli ni ya kikale au haiwezi kutumiwa tena? Sivyo hata kidogo.

Kuna wanaume na wanawake, vijana kwa wazee, hesabu yao ikifikia mamilioni, wanaojua kwamba Biblia ni chanzo cha msaada wenye thamani kubwa sana. Ni kama vile dibaji ya Today’s English Version husema: “Biblia si fasihi nzuri sana tu ya kusifiwa na kustahiwa; ni Habari Njema kwa watu wote kila mahali—ujumbe upaswao kueleweka na kutumiwa katika maisha ya kila siku.”

Gospeli inamaanisha nini kwako? Je! wewe huitumia kuwa mwongozo katika maisha yako ya kila siku? Ona vile habari njema zilivyonufaisha baadhi ya wale waliozisikiliza katika karne ya kwanza na jinsi ambavyo wengine wamenufaika katika wakati wetu.

Watu Waliosaidiwa na Gospeli

Katika siku ya Yesu watu mmoja mmoja kama vile wavuvi na wake wa nyumbani wenye bidii walivutwa na habari njema na walijifunza kweli juu ya kusudi la Mungu kwa mwanadamu. Habari njema zilibadili maisha zao sana na mara nyingi ziliwaletea kitulizo kingi sana. Kwa kielelezo, Mariamu Magdalene aliponywa na upagazi wa roho waovu. Zakayo, aliyekuwa mtoza kodi mkuu wakati mmoja, aliacha njia yake ya maisha yenye pupa. (Luka 8:2; 19:1-10) Vipofu na wenye ukoma walisaidiwa walipomjia Yesu, yule aliyekuwa akihubiri habari njema. (Luka 17:11-19; Yohana 9:1-7) Yesu angeweza kusema kwa haki hivi: “Vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.”—Mathayo 11:5.

Lakini, jambo la maana zaidi ya kuponywa kwao, lilikuwa njia ambayo hizo habari njema zilivyobadili utu wa wengi wa wale mmoja mmoja waliopungukiwa. Wale wenye mioyo myeupe walijazwa na tumaini la wakati ujao. Waliweka tumaini lao katika Ufalme wa Mungu—jambo lililo bora kuliko gospeli yoyote ya kijamii. (Mathayo 4:23) Tumaini lao halikufadhaishwa na kifo cha Yesu. Likieleza mambo hata baada ya tukio hilo, Matendo 5:42, linasema hivi juu ya wanafunzi wake: “Kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao [nyumba kwa nyumba, NW] hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.” Katika karne ya kwanza, watu katika mabara mengi walipokea msaada wa kiroho kwa sababu waliitikia kuhubiri kwa jinsi hiyo.

Ufalme ulikuwa ndio habari njema zaidi wakati huo wa nyuma. Je! ujumbe wa Ufalme ungali habari njema?

Habari Njema Humaanisha Nini Leo?

Ikiwa unatamani ulimwengu wenye amani, ulio salama, basi kwa hakika habari juu ya Ufalme ni nzuri. Kwa kweli, katika ulimwengu wenye mamia ya mamilioni ya watu wasio na chakula cha kutosha na wenye kufa njaa, ulimwengu wenye magonjwa yenye kuhofisha yanayotisha kila mtu, wenye uhalifu unaoongezeka kwa njia yenye kuhofisha, na wenye hali ya kisiasa isiyo na uthabiti, hizo ni habari njema pekee za kweli na zenye kudumu. Zinawakilisha tumaini pekee la maendeleo ya kweli.

Hiyo ndiyo sababu Yesu alitoa unabii huu kuhusu siku yetu: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Maneno hayo yanatimizwa katika njia ya ajabu huku Mashahidi wa Yehova wahubiripo habari njema katika mabara zaidi ya 200. Kichapo cha Katoliki, Nova Evangelização 2000, kinawapongeza Mashahidi kwa hilo, kikisema hivi: “Tunawapata Mashahidi wa Yehova wapi? Kwenye milango ya nyumba. Na ili kuwa Shahidi wa Yehova, zaidi ya kuwa mali ya Yehova, mtu anapaswa awe shahidi. Kwa hiyo, tunawaona wakifanya kazi, wakitangaza, wakitoa, yale ambayo wamejionea wenyewe.”

Hata hivyo, hakuna yeyote anayenufaika kutokana na habari njema vivi hivi tu. Zitasaidia wale tu wanaosikiliza na kutii. Ili kuonyesha jambo hilo, Yesu alitoa mfano juu ya mtu aliyeenda kupanda mbegu. Udongo wa aina tofauti-tofauti ambao mbegu iliangukia ulitoa kielezi cha hali ya moyo ya aina tofauti-tofauti inayoonyeshwa na wenye kusikia habari njema. Yesu alisema hivi: “Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake . . . Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; naye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.”—Mathayo 13:18-23.

Kama vile katika karne ya kwanza, watu wengi leo hawajitahidi sana kuzielewa habari njema. Hawapati kuzielewa, na hivyo hawapokei faida zazo. Wengine huonyesha uthamini kwa ajili ya habari njema na hujifunza jinsi ya kupatanisha maisha zao na mapenzi ya Mungu. Kwa njia hiyo wao hubarikiwa. Wewe ni wa kikundi kipi?

Nguvu ya Gospeli Leo

Maono hushuhudia kwamba kuzielewa habari njema husaidia wale ‘wasiokuwa na tumaini wala Mungu duniani.’ (Waefeso 2:12; 4:22-24) Roberto kutoka Rio de Janeiro alihitaji msaada. Tangu ujana wake, alikuwa amekuwa na njia ya maisha ya ufasiki, akiwa amejihusisha na dawa za kulevya, ukosefu wa maadili, na wizi. Mwishowe alifungwa gerezani. Alipokuwa huko Roberto alijifunza Biblia pamoja na Shahidi aliyekuwa akitembelea. Alifanya maendeleo vizuri sana kiroho hivi kwamba muda wake gerezani ukapunguzwa sana.

Baada ya kuachiliwa, Roberto alikutana na msichana mchanga ambaye alikuwa amemshambulia na kumtisha kwa bunduki wakati mmoja. Yeye pia alikuwa akijifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ni nini kilichotukia? Ifuatayo ni sehemu ya barua inayosimulia tukio hilo: “Walikutana katika Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza baada ya shambulio hilo. Mkutano huo ulikuwa wenye kugusa moyo. Wote wawili walitokwa na machozi ya kihisiamoyo wakakumbatiana wakiwa ndugu na dada. Sasa yule aliyekuwa mwizi pamoja na yule aliyeshambuliwa wote wanamsifu Yehova.”

Mwanamke mwingine, Isabel, alihitaji msaada pia, kwani alijulikana kwa wepesi wake wa kukasirika. Alikuwa amejihusisha sana na uwasiliani-roho na uchawi na alikuwa akiteswa na roho waovu. Alipokuwa akijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, aliona kwamba habari njema zilimsaidia kwelikweli. Baada ya muda fulani, alijiweka huru na udhibiti wa roho waovu akabadili utu wake—mwishowe akijifunza kuthibiti hasira yake. Sasa yeye ni Mkristo mwaminifu, anayejulikana kuwa mtu mwenye fadhili katika kushughulika na wengine.

Naam, habari njema si nadharia tu. Zina nguvu ya kubadili maisha. (1 Wakorintho 6:9-11) Zinafanya hata zaidi ya hayo. Zinaelekeza pia kwenye baraka za wakati ujao.

Baraka Zilizoko Mbele Bado

Kulingana na Neno la Mungu, wakati ujao una matarajio mazuri ajabu. Tutaona utimizo wa sala ya Yesu ya kuomba Ufalme wa Mungu uje na mapenzi Yake yatimizwe hapa duniani kama ilivyo huko mbinguni. (Mathayo 6:9, 10) Hivi karibuni, mfumo wa mambo uliopo ukiwa na ufisadi na jeuri yenye kushusha moyo utaondolewa, na serikali ya Mungu ya kimbingu, Ufalme wake, utatawala juu ya watu mmoja mmoja wenye moyo ufaao waliokuwa na nia ya kusikiliza na kutii habari njema.—Danieli 2:44.

Maendeleo makubwa sana yatafuata huku wanadamu waaminifu wanapoelekezwa ili kuibadili dunia iwe paradiso ambapo watu wasikivu wataishi milele. (Zaburi 37:11, 29) Kwa hakika, ni habari njema kwamba uhalifu, ugonjwa, njaa kuu, uchafuzi, na vita vitatokomea milele! Je! wewe waweza kujiona mwenyewe na familia yako mkiishi katika ulimwengu huo mpya katika amani na afya kamilifu bila hofu ya ugonjwa au kifo?—Ufunuo 21:4.

Ni kweli, wengi huziona habari hizo njema kuwa ni kurahisisha mambo au kuwa mawazio-wazio tu. Lakini wanakosea. Habari njema zinategemea ushuhuda wenye uthabiti zaidi, na tayari zimebadili mamilioni ya maisha. Kwa hiyo, usishawishwe kamwe ikiwa wengine hawaamini.

Wazia mtu mwenye busara anayenunua shamba katika eneo lenye kusitawi, akitumaini kupata faida kutokana na pato lake. Je! mtu yeyote angemlaumu kwa kutumia pesa zake kwa njia hiyo ili kupata faida? La. Yaelekea zaidi kwamba, watu wangesema alikuwa akitenda kwa hekima. Basi, kwa nini usiwe mwenye kutazamia ya mbele kwa habari ya Ufalme na kupata faida kutokana na habari njema? Kwa kuwa kukubali habari njema kunamaanisha wokovu, hakuna pato jingine lolote litakaloleta faida zaidi.—Warumi 1:16.

Unaweza kupataje faida kutokana na habari njema? Kwanza, uwe na nia ya kufundishwa na Mungu. Halafu tenda kulingana na yale umejifunza. Fuata matakwa ya msingi, kama yalivyoorodheshwa na nabii Mwebrania mmoja wa kale: “BWANA [Yehova, NW] anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!” (Mika 6:8) Kujifunza jinsi ya kwenda na Mungu huchukua wakati na bidii. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova, waliowasaidia Roberto na Isabel, watafurahi kukusaidia katika habari hiyo—kama vile ambavyo wamesaidia mamilioni ya wengine muda wa miaka iliyopita.

Unapongojea utimizo wa ahadi za Mungu, tunza pato lako kwa kuishi kulingana na habari njema, ukifurahia amani ya akili na kujenga uhusiano wa karibu zaidi na Mungu. Pato lako litakuwa salama—hakuna mshuko wowote wa kiuchumi au mchafuko wa kisiasa utakaolitisha. Na mwishowe, litakuletea faida nzuri ajabu. Faida hiyo ni nini? Mtume Yohana aliandika hivi: “Dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.”—1 Yohana 2:17.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Mbegu za habari njema huangukia udongo wa aina tofauti-tofauti

[Hisani]

Garo Nalbandian

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki