Ukumbusho—Sherehe ya Kikristo
1 Yesu alianzisha Ukumbusho mnamo Nisani 14, 33 W.K., naye akaagiza mitume wake hivi: “Endeleeni kufanya hivi katika ukumbusho wangu.” (Luka 22:19, NW) Mtume Paulo alieleza kwamba kwa kufanya hivyo ‘mnaendelea kupiga mbiu ya kifo cha Bwana, hadi atakapowasili.’ (1 Kor. 11:26, NW) Inafaa kukumbuka kifo cha Yesu kwa sababu ya yote ambayo kinatimiza katika kutekelezwa kwa kusudi la Yehova. Dhabihu ya ukombozi inaandaa msingi wenyewe kwa ajili ya imani yetu na hutupa sisi tumaini la maisha ya wakati ujao.
2 Tangu mwanzo wa kundi la Kikristo, wanafunzi wa Yesu wamesherehekea kwa uaminifu Ukumbusho wa kifo chake. Katika nyakati za kisasa iliripotiwa mapema 1899 kwamba 2,501 katika United States walishiriki katika sherehe ya Ukumbusho. Sasa, miaka 91 baadaye, Nisani 14 itakuwa mnamo Jumanne, Aprili 10, baada ya jua kushuka, na watu karibu arobaini elfu katika Afrika Mashariki wanatazamiwa kuadhmisha sherehe hii ya kila mwaka.
MATAYARISHO YANAHITAJI KUFANYWA NA WAZEE
3 Kwa sababu ya umaana wa pindi hii na hudhurio kubwa linalotarajiwa, makundi hufanya matayarisho ya kimbele. (1 Kor. 14:40) Desturi na kufanya mambo kirasmi mno havihusiki. Sivyo, kwa maana kwenye Mathayo 26:26-30 tunaona usahili ambao Yesu alianza sherehe hii ya maana. (1 Kor. 11:23-26) Lakini mambo fulani yaliyo ya muhimu yafuatwe ikiwa Ukumbusho utasherehekewa kisahihi. Hiyo ni kutia na nini?
4 Kati ya mambo mengine, wazee wanahakikisha kwamba heshima inaonyeshwa kwa ajili ya Chakula cha Jioni cha Bwana kwa kuwa na mifano ya aina inayofaa. Mkate usiotiwa chachu, kama vile matzoth wa Kiyahudi usiotiwa kikolezo, uliotengenezwa kwa unga wa ngano na maji tu waweza kutumiwa. Pia ni divai ya zabibu nyekundu tu ambayo haijaghoshiwa (isiyochanganywa na kitu), kama vile Chianti, Burgundy, au claret mojawapo, ndiyo yapasa kutumiwa. Divai nyekundu iliyochanganywa nyumbani yaweza kutumiwa ikiwa haijatiwa sukari, kikolezo, au kuongezwa kitu.
5 Pia wazee watataka kuchagua ndugu ambao ni kielelezo kizuri na wanaostahili vizuri, yafaa wazee au watumishi wa huduma, wapitishe mifano. Wanapaswa kuwa na utaratibu mzuri na wanapaswa kuelewa barabara mgawo wao unahusisha nini. Wale wanaotumikia kuwa wakaribishaji wapaswa kuelezwa juu ya wajibu wao, kama vile kuelekeza watu ndani na nje ya jumba na pia kuongoza motokaa zilizoongezeka. Hasa hilo ni jambo la maana katika visa ambavyo makundi kadhaa yatatumia Jumba la Ufalme au uwanja wa Jumba la Ufalme ule ule. Mipango yapasa pia kufanywa ili kuhakikisha kwamba mnenaji anataarifiwa vya kufaa juu ya wakati na mahali pa sherehe hiyo.—Kwa ajili ya vikumbusho vya ziada juu ya mambo ya kujitayarishia kwa ajili ya Ukumbusho, ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 15, 1985, ukurasa 17, na Februari 15, 1990, kurasa 16-18; Huduma ya Ufalme Yetu, Machi 1989, ukurasa 4.
MATAYARISHO YA KIBINAFSI
6 Sisi sote tunapaswa kujitahidi kutwaa manufaa kamili kutokana na sherehe hii iliyo takatifu zaidi. Kati ya mambo mengine, tunaweza kujitayarisha wenyewe kiakili kwa kufuatia sana usomaji wa Biblia kwa ajili ya Aprili 5-10, kama inavyoonyeshwa kwenye Kalenda ya 1990 ya Mashahidi wa Yehova. Pia, tunapaswa kufanya mipango ya kualika na kusaidia watu wengi iwezekanavyo ili wahudhurie pindi hii ya pekee sana. Na sisi tunapaswa kuwafanya wale wanaohudhuria wahisi wamekaribishwa.
7 Kwa matayarisho kamili ya kimbele, tutaonyesha kwamba tunaona kuhudhuria Ukumbusho kuwa pendeleo na nafasi ya kuonyesha uthamini wetu kwa ajili ya dhabihu ya Kristo. Sherehe ya Ukumbusho ya mwaka huu na ithibitike kuwa wakati wa kitia-moyo chenye kujenga kwa watumishi wote wa Yehova. Na itie ndani yetu sote roho ya itibari aliyoonyesha Yesu. Tegemeo letu katika Yehova litatusaidia tuushinde ulimwengu na kupokea zawadi zetu zihusuzo.—Yohana 16:33; 2 Pet. 1:10; Ufu. 7:9, 10, 14.