Wimbo 23
Tumaini la Biblia kwa Wanadamu
1. Giza titi; hofu nyingi
Na viumbe vina wasiwasi bila
Tumaini. Vyapapasa
Mwisho wakaribia.
Biblia yatutia moyo sana,
Kwa kuwa Ufalme si mbali sana.
Mungu atafuta machozi yote.
Iweni wima; musihofu kamwe.
2. Ni huzuni, hofu nyingi,
Ni wazi kabisa, watu wanakufa.
Wote mwisho kaburini;
Jasho la watu bure.
Biblia inatoa tumaini,
Kuna ufufuo wa watu wafu.
Na watapewa maji ya uzima.
Hizo ni habari njema za Mungu.
3. Kwa kiburi, wadhihaki
Wamusuta Mungu, wachezea dhambi.
Na Shetani atawala,
Uovu waenea.
Biblia yasema karibu kuwe
Hukumu ya Yehova duniani.
Waovu wafutwe kwa umilele,
Wapole wataijaza dunia.