Matangazo
◼ Toleo la Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, lengo likiwa kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Tutatoa kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Je, Kweli Mungu Anatujali?, Je, Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya. Huenda broshua zifuatazo zinafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je Ziko Kweli?
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Mnaweza kuomba fomu hizo kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni akiba ya angalau mwaka mmoja. Kabla ya kutuma ombi la painia wa kawaida kwenye ofisi ya tawi, hakikisheni kwamba limejazwa kwa usahihi.
◼ Ofisi ya tawi inapaswa kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kuna mabadiliko yoyote ya anwani ua namba za simu, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) na kuituma mara moja kwenye ofisi ya tawi. Pia fomu hiyo inapaswa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote ya namba ya simu ya eneo.
◼ Iwapo unapanga kutembelea nchi nyingine, na unataka kujua tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano au kusanyiko, unapaswa kuiuliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Kuna orodha ya anwani za ofisi ya tawi katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni.