Habari za Kitheokrasi
Ofisi za tawi zifuatazo ziliwekwa wakfu hivi karibuni.
Burundi: Ofisi mpya ya tawi na Jumba la Kusanyiko viliwekwa wakfu Jumamosi, Novemba 25, 2006 na Ndugu Guy Pierce wa Baraza Linaloongoza kukiwa na hudhurio la watu 1,141. Siku iliyofuata, Jumapili Novemba 26, 2006 kulikuwa na programu ya pekee katika Uwanja ulio jirani ambapo umati wa watu 5,679 walifurahia programu hiyo.
Rwanda: Ofisi mpya ya tawi iliwekwa wakfu Jumamosi, Desemba 2, 2006 na Ndugu Guy Pierce. Kulikuwa na watu 554 kwenye programu ya wakfu na umati wa watu 13,292 walihudhuria programu ya pekee siku iliyofuata, Jumapili Desemba 3, 2006 kwenye uwanja ulio karibu.
Uganda: Ofisi mpya ya tawi iliwekwa wakfu Januari 20, 2007 na Ndugu Anthony Morris wa Baraza Linaloongoza, kukiwa na hudhurio la watu 665. Kabla ya hotuba ya wakfu, mwangalizi wa eneo la dunia, Ndugu Leon Weaver Jr. kutoka Betheli ya Brooklyn, alitoa hotuba yenye kutia moyo yenye kichwa “Kutegemeza Kazi ya Yehova Inayozidi Kupanuka.” Siku iliyofuatia, Januari 21, 2007 kulikuwa na programu ya pekee iliyofanyika kwenye uwanja ulio katikati ya jiji. Watu 4,915 walihudhuria, yaani, zaidi ya watu 800 kuliko idadi ya wahubiri nchini Uganda!
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Burundi: Gitega Centre (Jumba la Ufalme la kwanza nchini Burundi linaloweza kutumiwa hata kwa makusanyiko), Mugerama, Ndaro, na Remba
Kenya: Kiritiri, Mutara, na Ndima-ini.
Uganda: Kyaka Bukere na Kyaka Mukondo.