Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/07 kur. 5-6
  • Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Tukiwa Mashahidi wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Tukiwa Mashahidi wa Yehova
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 4/07 kur. 5-6

Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Tukiwa Mashahidi wa Yehova

1 Tukiwa Mashahidi wa Yehova tuna pendeleo kubwa zaidi duniani. Tunamwakilisha Yehova katika kesi ya ulimwenguni pote inayowahusisha wote wanaoabudiwa kama miungu. (Isa. 41:1, 23; 43:12) Ili kutusaidia kutetea imani yetu kwa njia nzuri, Yehova ameandaa maktaba iliyo na vichapo vingi sana. (1 Pet. 3:15) Fahirisi ya Vichapo ni kitabu kizuri cha kupata habari tunayohitaji. Kufahamu vizuri habari fulani muhimu kunaweza kutusaidia kuwa stadi zaidi kukitumia.

2 Kila mmoja wetu anapaswa kufahamu vizuri kichwa kikuu “Yehova.” Chini ya kichwa hicho katika Fahirisi ya 2004, unaweza kupata marejeo yanayoeleza sababu ambayo Yehova ameruhusu mambo mabaya yatendeke kwa muda fulani. Pia utapata kichwa cha katikati “Jina” katika Fahirisi ya 1930-1985, Fahirisi ya 1986-2000 (za Kiingereza), ama Fahirisi nyingine ya karibuni. Marejeo kuhusu kila kitu ambacho kimechapishwa kuhusu jina Yehova yanapatikana hapo.

3 Kichwa kingine muhimu sana ni “Mashahidi wa Yehova.” Kina marejeo mengi kuhusu Mashahidi wa Yehova wakiwa tengenezo. Je, unajua maoni yetu ya kisheria kuhusu elimu ya juu, kuchunguza maiti, kuua ili kujilinda, au msaada wa umma? Utapata marejeo kuhusu maswali kama hayo chini ya kichwa kidogo “maoni yao kuhusu—.” Chini zaidi kuna historia ya Mashahidi wa Yehova wa leo, katika nchi mbalimbali, na unaweza kupata orodha ndefu ya maelezo kuhusu Mashahidi wa Yehova chini ya kichwa cha katikati “Maoni ya Watu Wasio Mashahidi.”

4 Masimulizi ya maisha ya watumishi waaminifu wa Yehova hututia moyo na kutufundisha. Yanaweza kutusaidia kuweka msingi imara wa wakati ujao kwa ajili ya watoto wetu na wanafunzi wa Biblia. Unaweza kupata masimulizi hayo ya maisha yaliyoorodheshwa kwa jina la watu wenyewe na kichwa cha makala chini ya kichwa “Masimulizi ya Maisha ya Mashahidi wa Yehova.” Vichwa vidogo vifuatavyo vitaonyesha jinsi kitabu Fahirisi kinavyoweza kutusaidia kutanikoni, katika familia, na shambani.

5 Kutanikoni. Kupitia Yesu Kristo, ambaye ni Kichwa cha kutaniko la Kikristo, Yehova amempa “msimamizi-nyumba” madaraka. (Luka 12:42, 43) Mpango huo umefanya tuweze kupokea mwelekezo uliochapishwa wa jinsi ‘tunavyopaswa kujiendesha katika nyumba ya Mungu.’ (1 Tim. 3:15) Kifaa chetu kikuu cha kutafuta kile ambacho kimechapishwa ni Fahirisi ya Vichapo. Kinaweza kukusaidiaje?

6 Je, wewe ni mzee? Kuna vichwa viwili ambavyo vina habari kuhusu madaraka yako: “Wazee Wakristo” na “Waangalizi.” Sehemu yenye kichwa “Wazee” ina marejeo mengi yenye habari kuhusu jinsi ya kuwasaidia watu mbalimbali kutanikoni, jinsi ya kutoa mashauri, uhusiano ndani ya baraza la wazee, madaraka ya wazee, na kadhalika. Marejeo kuhusu sifa za ustahili yanapatikana chini ya kichwa “Waangalizi,” kwa kuwa neno hilo ndilo hutumiwa katika Biblia kuzungumzia habari hiyo. Pia kuna vichwa vikuu kuhusu migawo rasmi kama vile “Mwangalizi-msimamizi,” “Mwangalizi wa utumishi,” na “Mwandishi.” Pia, kichwa kikuu “Makutaniko” kina habari muhimu.

7 Nyinyi watumishi wa huduma mnatimiza jukumu la maana katika kutaniko. Kichwa “Watumishi wa Huduma” kinaorodhesha habari kuhusu sifa zenu za ustahili na madaraka yenu. Pia utapata marejeo ya habari kuhusu umuhimu wa migawo ya utumishi ambayo unaweza kufikia na jinsi unavyoweza kufikia madaraka mengine.

8 Nufaisha Familia. Ikiwarejezea washiriki wa familia, 1 Timotheo 5:4 inasema: “Acha hao wajifunze kwanza kuzoea ujitoaji-kimungu nyumbani kwao wenyewe.” Kwa kweli, tunapaswa kujifunza kuzoea ujitoaji-kimungu tunaposhughulika na washiriki wa familia. Ili kufanya hivyo tunahitaji mwongozo wa kimungu, kwa kuwa kutunza washiriki wa familia ni sehemu ya daraka letu la Kikristo. Fahirisi ya Vichapo inaweza kutusaidia kupata mwongozo wa kushughulikia hali mbalimbali zinazotukia katika maisha ya familia.

9 Familia huanzishwa mwanamume na mwanamke wanapooana. (Mwa. 2:24) Je, unafikiria kufunga ndoa? Chini ya kichwa “Ndoa,” utapata kichwa kidogo “kuchagua mume au mke.” Pia Fahirisi ina vichwa vidogo vyenye kichwa “kuimarisha ndoa” “yenye furaha” na “uaminifu katika ndoa.” Kila moja kati ya vichwa hivyo ina marejeo ya habari ambazo zitawasaidia wanaotaka kufunga ndoa na wale ambao tayari wamefunga ndoa. Isitoshe, katika Fahirisi ya Kiingereza vichwa vidogo kama vile “communication,” “closeness in,” na “peace” huelekeza mtu kwenye habari inayoweza kuboresha ndoa. Hali ngumu zinapotokea, kichwa kidogo “problems in” kinaweza kukuelekeza kwenye mashauri yanayofaa kuhusu jinsi ya kusuluhisha matatizo katika ndoa.

10 Watoto ni urithi kutoka kwa Yehova. (Zab. 127:3) Wazazi wanaweza kuwaleaje watoto wao “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova”? (Efe. 6:4) Mwongozo ambao Yehova anatoa kupitia Neno lake na jamii ya mtumwa mwaminifu ni wenye thamani sana. Wazazi wanahitaji kuelewa vizuri hisia na mahitaji ya watoto wao. Mashauri na mapendekezo yenye manufaa yanaweza kupatikana kupitia Fahirisi chini ya vichwa “Watoto” na “Vijana.” Na vipi kuhusu kukazia sheria ya Yehova ndani ya mioyo yao michanga? Kichwa “Watoto, Kuwalea” kina habari muhimu kuhusu kila jambo linalohusu kuwalea watoto, kutia ndani jinsi ya kuwasaidia kusitawisha uhusiano wa kibinafsi na Yehova na kukuza tamaa kwa ajili ya kweli. (1 Pet. 2:2) Mazungumzo ya Biblia ya familia yaliyopangwa mapema ni muhimu ili kufanikisha familia. (Kum. 6:6-9; Isa. 54:13; Efe. 5:25, 26) Chini ya kichwa hicho unaweza kupata marejeo kuhusu mapendekezo ya kuwa na mazungumzo ya familia yenye kufurahisha, kama vile chini ya kichwa kidogo “kuwasaidia” kuna kichwa kidogo “kufurahia kujifunza.”

11 Shambani. Upendo wetu kwa Yehova na jirani hutuchochea kuhubiri habari njema za Ufalme. Kwa kushughulika na kweli kwa ustadi, tunaweza kupindua “mawazo na kila jambo lililo juu sana ambalo limeinuliwa kinyume cha ujuzi wa Mungu.” (2 Kor. 10:5) Fahirisi ya Vichapo imekusudiwa kutusaidia kufanya hivyo.

12 Kichwa kikuu cha marejeo yanayohusu utendaji wetu wa kuhubiri ni “Huduma ya Shambani.” Kila jambo linapatikana humo, kutia ndani, mtazamo wetu, utangulizi, kukabiliana na vipingamizi, mapendekezo ya kutoa vichapo mbalimbali, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia. Je, ungependa kutoa mfano kwa kutumia mambo fulani yaliyoonwa? Unaweza kupata unachohitaji chini ya kichwa kikuu “Mambo Yaliyoonwa Katika Huduma ya Shambani.”

13 Je, unatamani kuanzisha funzo la Biblia? Au je, una funzo ambalo halifanyi maendeleo? Chini ya kichwa kikuu “Mafunzo ya Biblia” kuna vichwa vidogo vyenye marejeo ya kukusaidia kupata na kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo kama vile “kufundisha kwenye.”

14 Kutimiza huduma yetu ya Ufalme huleta uradhi mwingi. (Yoh. 4:34) Fahirisi ya Vichapo inaweza kukusaidia unaposhiriki katika kazi hii yenye shangwe na katika sehemu nyingine za maisha ya Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki