Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 30, 2007. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 5 hadi Aprili 30, 2007. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali. utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kufanya nini ili muhtasari wetu wa hotuba uwe rahisi? [be uku. 168 fu. 4]
2. Taja njia nne tunazoweza kutumia ili habari yetu ifuatane vizuri. [be uku. 170 fu. 3–uku. 172 fu. 4]
3. Tunapaswa kufikiria mambo gani tunapochagua habari tutakayotumia katika hotuba yetu? [be uku. 173 fu. 1-2]
4. Taja baadhi ya faida za kutoa hotuba bila kutazama sana maandishi. [be uku. 175 fu. 2-4]
5. Kwa nini ni muhimu kutoa hotuba kwa njia ya maongezi, na tunaweza kukuzaje sifa hii? [be uku. 179 fu. 4, sanduku; uku. 180, sanduku]
HOTUBA NA.1
6. Ndugu anapaswa kutayarishaje mambo makuu ya usomaji wa Biblia wa juma? [be uku. 47 fu. 3-4]
7. Ni jambo gani lililo muhimu zaidi kuhusu fidia ya Kristo kuliko faida ambazo tunapata kupitia hiyo fidia? [w05 11/1 uku. 14 fu. 1]
8. Maandiko yaliyoonyeshwa kwenye muhtasari wa hotuba ya watu wote yanapaswa kutumiwaje? [be uku. 53 fu. 1-2]
9. Yesu alikuwa na mradi gani alipokuwa akifundisha, nasi tunaweza kumwigaje? [be uku. 57 fu. 1]
10. Kwa nini kupambanua mambo ni njia nzuri ya kufundisha? [be uku. 57 fu. 3-4]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Tunaweza kujitahidije kufuata shauri la Yeremia 6:16 la kutembea katika “barabara za zamani za kale, mahali ambapo sasa pana njia nzuri”?
12. Kwa nini Yehova alichagua mfano wa korongo ili kuwafundisha Wayahudi wasio waaminifu, nasi tunajifunza nini? (Yer. 8:7)
13. Andiko la Yeremia 15:17 linapaswa kuathirije maoni yetu kuhusu vitumbuizo leo?
14. Wanadamu ni kama udongo mkononi mwa Mfinyanzi Mkuu, Yehova, katika njia gani? (Yer. 18:5-11)
15. Jinsi mataifa yanavyoorodheshwa kwenye Yeremia 25:17-26 kuna maana gani leo?