Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Agosti 15 na Amkeni! la Agosti. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mzee. Kwa kadiri wakati unavyoruhusu, soma na uzungumzie maandiko yaliyotajwa.
Dak. 20: “Fuata Kielelezo Kilichowekwa na Yesu.”a Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamefaidika kutokana na mfano mzuri wa wengine.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Tulifanya Nini Mwaka Uliopita? Mwangalizi wa utumishi anapitia mwaka wa utumishi uliopita, akikazia mambo mazuri yaliyotimizwa katika utumishi. Toa pongezi inayofaa. Taja jambo moja au mawili yanayohitaji kuzingatiwa katika mwaka mpya wa utumishi. Taja mambo fulani kuhusu utendaji wa mapainia ukiwapongeza kwa kazi yao nzuri. Eleza matokeo mazuri ambayo yamepatikana katika kuwasaidia wasiotenda.
Dak. 20: Undugu Wenye Umoja. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea sura ya 16 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Wimbo 74 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Tumia Trakti Kujua Biblia Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mwezi wa Oktoba. Toleo la Oktoba ni magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa upendezi unaonyeshwa, trakti Kujua Biblia inaweza kutumiwa kuanzisha funzo la Biblia. Zungumzia trakti hiyo kwa ufupi baada ya kuwaomba wakaribishaji wampe kila mmoja trakti hiyo, ikiwa zinapatikana. Eleza kwamba trakti hiyo inaweza kuzungumziwa yote au sehemu yake katika ziara ya kwanza au unaporudi. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa magazeti ya karibuni. Katika onyesho moja, mhubiri anamwachia trakti mwenye nyumba anayekataa magazeti. Katika onyesho la pili, mwenye nyumba anakubali magazeti, naye mhubiri anampa trakti hiyo, anazungumzia ukurasa wa 5, kisha anamwonyesha sehemu iliyo na picha ya kitabu Biblia Inafundisha kwenye ukurasa wa 6, na anaahidi kurudi na kitabu hicho.
Wimbo 222 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za mwezi wa Septemba.
Dak. 15: Barua Kutoka Ofisi ya Tawi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea barua kwenye ukurasa wa kwanza wa Huduma Yetu ya Ufalme. Waombe wasikilizaji waeleze mambo yaliyoonwa wakati wa kampeni ya kuwakaribisha watu wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Mfuateni Kristo!”
Dak. 20: “Kufanya Mengi Zaidi Katika Huduma Yetu.”b Tia ndani maelezo kutoka kwa ndugu na dada ambao wamejitahidi kufanya mengi zaidi katika huduma, waombe waeleze jinsi wanavyotafuta njia za kuongeza huduma yao. Unaweza kupanga mapema ili mhubiri mmoja au wawili watoe maelezo kuhusu jambo hilo.
Wimbo 102 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.