Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/07 kur. 3-6
  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2008

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2008
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Vichwa vidogo
  • Maagizo
  • RATIBA
Huduma ya Ufalme—2007
km 10/07 kur. 3-6

Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2008

Maagizo

Katika mwaka wa 2008, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kwa kutegemea utaratibu ufuatao.

VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Toleo la 1992) [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Toleo la 2004) [rs].

Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI kwa wimbo, sala, na utangulizi wa kuwakaribisha wasikilizaji. Kisha fuateni utaratibu ufuatao. Baada ya kila hotuba mwangalizi wa shule atamkaribisha msemaji anayefuata.

SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri-msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, watumishi wa huduma wanaostahili wanaweza kutumiwa.)

HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma anayestahili, nayo itategemea kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hotuba hii ya maagizo itolewe kwa dakika kumi. Lengo la kutoa hotuba hii si kuzungumzia tu habari, bali ni kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani, na kukazia mambo ambayo yatanufaisha kutaniko. Kichwa kilichoonyeshwa ndicho kinachopaswa kutumiwa. Inatarajiwa kwamba ndugu wanaopewa hotuba hii watazingatia wakati ulioonyeshwa. Ndugu anaweza kushauriwa faraghani inapohitajika.

MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee, au mtumishi wa huduma, anayestahili, atumie dakika tano za kwanza kutoa habari hiyo kwa njia itakayofaidi kutaniko. Anaweza kuzungumzia sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Hapaswi kutoa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye manufaa na jinsi inavyowanufaisha. Msemaji anapaswa kuwa mwangalifu asipite zile dakika zake tano za kwanza. Anapaswa kuhakikisha kwamba anawaachia wasikilizaji dakika tano ili watoe maelezo yao. Wasikilizaji wanapaswa kuombwa watoe maelezo mafupi (yasiyozidi sekunde 30) kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia na manufaa yake. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu waondoke.

HOTUBA NA. 2: Isizidi dakika 4. Hii ni hotuba ya usomaji inayopaswa kutolewa na ndugu. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari hiyo bila kutoa utangulizi wala umalizio. Mwangalizi wa shule atajitahidi hasa kuwasaidia wanafunzi wasome kwa njia inayoeleweka, wawe na ufasaha, wakazie maana kwa njia inayofaa, wawe na ubadilifu wa sauti, watue kwa njia inayofaa, na wasome kwa njia ya maongezi ya kawaida.

HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Hotuba hii inapaswa kutolewa na akina dada. Akina dada wanaopewa mgawo huu watapewa au watajichagulia kikao katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani katika eneo lenu. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Wanafunzi wapya wapewe hotuba zilizo na marejeo. Mwangalizi wa shule ataangalia hasa jinsi mwanafunzi anavyoeleza habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na mambo makuu. Mwangalizi wa shule atampa msaidizi mmoja.

HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kuzungumzia kichwa kilichoonyeshwa. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Ndugu anapopewa hotuba hii, ataitoa kama hotuba kwa wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa hotuba hii, ataitoa jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Mwangalizi wa shule anaweza kumpa ndugu Hotuba Na. 4 wakati wowote anapoona inafaa kufanya hivyo. Hakikisha kwamba akina ndugu tu ndio wanaopewa hotuba zenye vichwa vilivyo na alama ya nyota. Ikiwa mna wazee na watumishi wa huduma wengi katika kutaniko lenu wanaoshughulikia sehemu mbalimbali katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi, basi inapendekezwa kwamba vichwa vilivyo na alama ya nyota vipewe mzee au mtumishi wa huduma inapowezekana.

SHAURI: Dakika 1. Mwangalizi wa shule hatatangaza mapema sifa ya usemi ambayo mwanafunzi anafanyia kazi. Baada ya kila Hotuba Na. 2, Na. 3, na Na. 4, mwangalizi wa shule atatoa maelezo yanayojenga kuhusu jambo linalostahili kusifiwa katika hotuba hiyo. Lengo lake si kutoa pongezi tu, bali ni kuonyesha sababu hususa zilizofanya jambo fulani liwe zuri katika hotuba. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, mashauri mengine yanaweza kutolewa faraghani baada ya mkutano au katika pindi tofauti ili kumsaidia mwanafunzi afanye maendeleo.

WAKATI: Hotuba wala maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupita wakati. Wanafunzi wanaotoa Hotuba Na. 2 hadi 4, wanapaswa kukatizwa kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia wakipita wakati, wanapaswa kushauriwa faraghani. Wote wanapaswa kufuata wakati. Programu nzima: Dakika 45, bila kutia ndani wimbo na sala.

FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu cha shule.

MSHAURI MSAIDIZI: Mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kuchagua mzee mwenye uwezo, ikiwa yupo, awe mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee kadhaa kutanikoni, kila mwaka, mzee tofauti anayestahili anaweza kupewa mgawo huo. Mshauri msaidizi ana daraka la kuwashauri faraghani akina ndugu wanaotoa Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, inapohitajiwa. Hahitaji kuwashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo.

PITIO LA SHULE YA HUDUMA YA KITHEOKRASI: Dakika 30. Baada ya kila miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio. Sehemu hiyo itafanywa baada ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama inavyoonyeshwa juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio. Ikiwa kutaniko lenu lina kusanyiko la mzunguko katika juma la Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mtafanya pitio (na pia sehemu zile nyingine za juma hilo) juma litakalofuata, nazo sehemu zilizo katika ratiba ya juma hilo linalofuata zitatolewa katika kusanyiko hilo la mzunguko. Ikiwa mwangalizi wa mzunguko anatembelea kutaniko lenu katika juma la pitio, wimbo, hotuba ya sifa ya usemi, na mambo makuu ya usomaji wa Biblia zinapaswa kutolewa kama ilivyoonyeshwa katika ratiba. Hotuba ya maagizo (ambayo itatolewa baada ya hotuba ya sifa ya usemi) inapaswa kuwa ile ya juma litakalofuata. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya juma litakalofuata itaanza na hotuba ya sifa ya usemi kisha mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama ilivyoonyeshwa katika ratiba, na hatimaye pitio.

RATIBA

Jan. 7 Usomaji wa Biblia: Mathayo 1-6 Wimbo 62

Sifa ya Usemi: Kueleza Mambo Magumu (be uku. 228 ¶2-3)

Na. 1: Utangulizi wa Mathayo (si uku. 175-177 ¶1-10)

Na. 2: Mathayo 5:1-20

Na. 3: Kwa Nini Wanadamu Hufa? (rs uku. 100-101 ¶6)

Na. 4: Jinsi Roho Takatifu ya Mungu Inavyotusaidia

Jan. 14 Usomaji wa Biblia: Mathayo 7-11 Wimbo 224

Sifa ya Usemi: Jinsi Moyo Unavyohusika (be uku. 228 ¶4–uku. 229 ¶1)

Na. 1: Furahia Neno la Mungu (be uku. 9 ¶1-5)

Na. 2: Mathayo 10:1-23

Na. 3: Kuna Faida ya Kuwa Mnyoofu

Na. 4: Wafu Wako Wapi, na Wako Katika Hali Gani? (rs uku. 101 ¶7–uku. 103 ¶4)

Jan. 21 Usomaji wa Biblia: Mathayo 12-15 Wimbo 133

Sifa ya Usemi: Kuwaelimisha Wasikilizaji (be uku. 230 ¶1-6)

Na. 1: Soma Biblia Kila Siku (be uku. 10 ¶1–uku. 12 ¶3)

Na. 2: Mathayo 14:1-22

Na. 3: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawashiriki Katika Desturi za Kimapokeo za Kuomboleza? (rs uku. 104 ¶1–uku. 105 ¶2)

Na. 4: Mpinga-Kristo Ni Nani?

Jan. 28 Usomaji wa Biblia: Mathayo 16-21 Wimbo 176

Sifa ya Usemi: Kufanya Hotuba Iwe Yenye Kuelimisha kwa Kufanya Utafiti (be uku. 231 ¶1-3)

Na. 1: ‘Kazia Uangalifu Jinsi Unavyosikiliza’ (be uku. 13 ¶1–uku. 14 ¶5)

Na. 2: Mathayo 17:1-20

Na. 3: Kujibu Maoni Yenye Makosa Kuhusu Kifo (rs uku. 105 ¶3–uku. 106 ¶1)

Na. 4: Mambo Ambayo Wakristo Huyaona Kuwa Matakatifu

Feb. 4 Usomaji wa Biblia: Mathayo 22-25 Wimbo 151

Sifa ya Usemi: Kufafanua Maandiko (be uku. 231 ¶4-5)

Na. 1: Kuwa Wasikivu Mikutanoni na Makusanyikoni (be uku. 15 ¶1–uku. 16 ¶5)

Na. 2: Mathayo 23:1-24

Na. 3: Uzima wa Milele Hautachosha

Na. 4: Ndoto—Zilizoongozwa na Roho ya Mungu na Zile Ambazo Hazikuongozwa Nayo (rs uku. 232-233 ¶5)

Feb. 11 Usomaji wa Biblia: Mathayo 26-28 Wimbo 110

Sifa ya Usemi: Kufafanua Maneno (be uku. 232 ¶1)

Na. 1: Mathayo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 180-181 ¶29-33)

Na. 2: Mathayo 27:1-22

Na. 3: Kwa Nini Kuwa na Imani Kunahusisha Mengi Zaidi ya Kuamini Tu Kwamba Kuna Mungu?

Na. 4: Wakristo Hawapaswi Kutumia Dawa za Kulevya (rs uku. 48-50 ¶1)

Feb. 18 Usomaji wa Biblia: Marko 1-4 Wimbo 167

Sifa ya Usemi: Kusababu Kuhusiana na Maandiko (be uku. 232 ¶2-4)

Na. 1: Utangulizi wa Marko (si uku. 181-183 ¶1-11)

Na. 2: Marko 2:1-17

Na. 3: Kwa Nini Wakristo Hawatumii Bangi? (rs uku. 50 ¶2–uku. 51 ¶2)

Na. 4: Jinsi Upendo Unavyoimarisha Uhodari

Feb. 25 Usomaji wa Biblia: Marko 5-8 Wimbo 72

Sifa ya Usemi: Kuchagua Habari Zitakazowafaidi Wasikilizaji Wako (be uku. 232 ¶5–uku. 233 ¶4)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Mac. 3 Usomaji wa Biblia: Marko 9-12 Wimbo 195

Sifa ya Usemi: Kutumia Habari Ambazo Umepewa (be uku. 234 ¶1–uku. 235 ¶3)

Na. 1: Unaweza Kuboresha Kumbukumbu Yako (be uku. 17 ¶1–uku. 19 ¶1)

Na. 2: Marko 11:1-18

Na. 3: Kwa Nini Mungu Hawezi Kusema Uwongo?

Na. 4: Kwa Nini Wakristo Hawavuti Sigara? (rs uku. 51 ¶3–uku. 53 ¶2)

Mac. 10 Usomaji wa Biblia: Marko 13-16 Wimbo 87

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Vizuri (be uku. 236 ¶1-5)

Na. 1: Marko—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 186 ¶31-33)

Na. 2: Marko 14:1-21

Na. 3: Unaweza Kushindaje Mazoea Mabaya? (rs uku. 53 ¶3–uku. 54 ¶2)

Na. 4: Kwa Nini “Ghadhabu ya Mwanadamu Haitokezi Uadilifu wa Mungu?” (Yak. 1:20)

Mac. 17 Usomaji wa Biblia: Luka 1-3 Wimbo 13

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Ili Kutokeza Mambo Muhimu (be uku. 237 ¶1-2)

Na. 1: Utangulizi wa Luka (si uku. 187-188 ¶1-9)

Na. 2: Luka 1:1-23

Na. 3: Kwa Nini “Imani Bila Matendo Haizai?” (Yak. 2:20)

Na. 4: Mataifa Hayatazuia Kusudi la Mungu Kuhusiana na Dunia Lisitimizwe (rs uku. 69-70 ¶6)

Mac. 24 Usomaji wa Biblia: Luka 4-6 Wimbo 156

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Ili Kusababu Juu ya Habari (be uku. 237 ¶3–uku. 238 ¶2)

Na. 1: Jinsi Roho ya Mungu Inavyotusaidia Kukumbuka Mambo (be uku. 19 ¶2–uku. 20 ¶3)

Na. 2: Luka 4:1-21

Na. 3: Je, Yehova Ataiharibu Dunia kwa Moto? (rs uku. 71 ¶1–uku. 72 ¶1)

Na. 4: Kumwogopa Mungu Kunaweza Kutuzuia Tusitende Dhambi

Mac. 31 Usomaji wa Biblia: Luka 7-9 Wimbo 122

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Ili Kutambua Hisia za Moyoni (be uku. 238 ¶3-5)

Na. 1: Kwa Nini Ujitahidi Kuwa Msomaji Mzuri? (be uku. 21 ¶1–uku. 23 ¶3)

Na. 2: Luka 7:1-17

Na. 3: Uthibitisho wa Kwamba Mungu Anatupenda na Anataka Tuwe na Furaha

Na. 4: Washiriki wa Yerusalemu Mpya Hawatarudi Duniani Baada ya Waovu Kuharibiwa (rs uku. 72 ¶2–uku. 73 ¶1)

Apr. 7 Usomaji wa Biblia: Luka 10-12 Wimbo 68

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Ili Kutia Mkazo (be uku. 238 ¶6-uku. 239 ¶1)

Na. 1: Jinsi ya Kujitahidi Kuwa Msomaji Mzuri (be uku. 23 ¶4–uku. 26 ¶5)

Na. 2: Luka 11:37-54

Na. 3: Je, Kusudi la Mungu kwa Dunia Limebadilika? (rs uku. 73 ¶2–uku. 74 ¶1)

Na. 4: Andiko la Ufunuo 17:17 Linamaanisha Nini?

Apr. 14 Usomaji wa Biblia: Luka 13-17 Wimbo 86

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Ili Kufichua Fikira Zisizofaa (be uku. 239 ¶2-4)

Na. 1: Jinsi ya Kujifunza (be uku. 27 ¶1–uku. 31 ¶2)

Na. 2: Luka 16:1-15

Na. 3: Tunajifunza Nini Kutokana na Sheria ya Mungu ya Kuokota Masalio? (Law. 19:9, 10)

Na. 4: Tunaweza Kuwatiaje Moyo Wagonjwa? (rs uku. 106-107¶3)

Apr. 21 Usomaji wa Biblia: Luka 18-21 Wimbo 182

Sifa ya Usemi: Tashbihi na Sitiari Zinazofundisha (be uku. 240 ¶1–uku. 241 ¶1)

Na. 1: Luka—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 192-193 ¶30-35)

Na 2: Luka 18:1-17

Na. 3: Tunaweza Kuwatiaje Moyo Waliofiwa? (rs uku. 107 ¶4-8)

No. 4: Kinachomaanishwa na Kuepuka Manung’uniko (Flp. 2:14)

Apr. 28 Usomaji wa Biblia: Luka 22-24 Wimbo 218

Sifa ya Usemi: Kutumia Mifano (be uku. 241 ¶2-4)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Mei 5 Usomaji wa Biblia: Yohana 1-4 Wimbo 31

Sifa ya Usemi: Mifano Katika Maandiko (be uku. 242 ¶1-2)

Na. 1: Utangulizi wa Yohana (si uku. 193-195 ¶1-9)

Na. 2: Yohana 3:1-21

Na. 3: Mambo Tunayojifunza Kutokana na Daudi Kukataa Mfalme Sauli Auawe

Na. 4: Kuwatia Moyo Wale Wanaoteswa kwa Kufanya Mapenzi ya Mungu (rs uku. 108 ¶1-6)

Mei 12 Usomaji wa Biblia: Yohana 5-7 Wimbo 150

Sifa ya Usemi: Je, Mfano Huo Unaeleweka? (be uku. 242 ¶3–uku. 243 ¶1)

Na. 1: Funzo Lina Faida (be uku. 31 ¶3–uku. 32 ¶3)

Na. 2: Yohana 6:1-21

Na. 3: Mambo Tunayojifunza Kutokana na Masimulizi Kuhusu Anania na Safira

Na. 4: Unaweza Kuwatiaje Moyo Wale Waliovunjika Moyo kwa Sababu ya Ukosefu wa Haki? (rs uku. 108 ¶7–uku. 109 ¶2)

Mei 19 Usomaji wa Biblia: Yohana 8-11 Wimbo 102

Sifa ya Usemi: Mifano ya Hali za Kawaida (be uku. 244 ¶1-2)

Na. 1: Jinsi ya Kufanya Utafiti kwa Kutumia Biblia (be uku. 33 ¶1–uku. 35 ¶2)

Na. 2: Yohana 11:38-57

Na. 3: Unaweza Kuwatiaje Moyo Wale Wanaokazwa Sana na Matatizo ya Kiuchumi? (rs uku. 109 ¶3-7)

Na. 4: Kwa Kuwa Haingewezekana Kumwadhibu Mtu Ambaye Hakutii Amri ya Kumi, Kwa Nini Ilitolewa?

Mei 26 Usomaji wa Biblia: Yohana 12-16 Wimbo 3

Sifa ya Usemi: Mifano Inayofaa Wasikilizaji Wako (be uku. 244 ¶3–uku. 245 ¶4)

Na. 1: Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti (be uku. 35 ¶3–uku. 38 ¶4)

Na. 2: Yohana 12:1-19

Na. 3: Kuwatia Moyo Watu Ambao Wamevunjika Moyo kwa Sababu ya Makosa Yao (rs uku. 109 ¶8–uku.110 ¶3)

Na. 4: Jinsi Tunavyomtupia Yehova Mzigo Wetu (Zab. 55:22)

Juni 2 Usomaji wa Biblia: Yohana 17-21 Wimbo 198

Sifa ya Usemi: Kutumia Vizuri Vielelezo (be uku. 247 ¶1-2)

Na. 1: Yohana—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 198-199 ¶30-35)

Na. 2: Yohana 21:1-14

Na. 3: Kwa Nini Tumwamini Mungu Ambaye Hatuwezi Kumwona?

Na. 4: Mageuzi—Fundisho Linalowatatanisha Wanasayansi (rs uku. 161-162 ¶4)

Juni 9 Usomaji wa Biblia: Matendo 1-4 Wimbo 92

Sifa ya Usemi Jinsi Yesu Alivyotumia Vielelezo (be uku. 247 ¶3)

Na. 1: Utangulizi wa Matendo (si uku. 199-200 ¶1-8)

Na. 2: Matendo 1:1-14

Na. 3: Fundisho la Mageuzi, Mabaki ya Viumbe vya Zamani, na Mambo Yanayopatana na Akili (rs uku. 162 ¶5–uku. 166 ¶1)

Na. 4: ‘Uhuru wa Kusema’ Unahusisha Nini? (Ebr. 3:6)

Juni 16 Usomaji wa Biblia: Matendo 5-7 Wimbo 2

Sifa ya Usemi: Njia za Kutumia Vielelezo (be uku. 248 ¶1-3)

Na. 1: Kutayarisha Muhtasari (be uku. 39-42)

Na. 2: Matendo 5:1-16

Na. 3: Kujibu Madai ya Watu Wanaoamini Mageuzi (rs uku. 166 ¶2–uku. 168 ¶2)

Na. 4: Kwa Nini Kumwogopa Yehova Ni Mwanzo wa Hekima? (Zab. 111:10)

Juni 23 Usomaji wa Biblia: Matendo 8-10 Wimbo 116

Sifa ya Usemi: Kutumia Ramani, Programu za Kusanyiko, na Video (be uku. 248 ¶4–uku. 249 ¶2)

Na. 1: Kutayarisha Migawo ya Shule (be uku. 43 ¶1–uku. 44 ¶3)

Na. 2: Matendo 8:1-17

Na. 3: Jinsi Yesu ‘Atakavyomkomboa Maskini’ (Zab. 72:12)

Na. 4: Kwa Nini Watu Wengi Hawana Imani? (rs uku. 91-uku. 92 ¶3)

Juni 30 Usomaji wa Biblia: Matendo 11-14 Wimbo 79

Sifa ya Usemi: Kutumia Vielelezo Mbele ya Watu Wengi (be uku. 249 ¶3–uku. 250 ¶1)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Julai 7 Usomaji wa Biblia: Matendo 15-17 Wimbo 203

Sifa ya Usemi: Kwa Nini Ni Muhimu Kusababu? (be uku. 251 ¶1-3)

Na. 1: Kutayarisha Ukifikiria Kichwa Kikuu na Kikao (be uku. 44 ¶4–uku. 46 ¶2)

Na. 2: Matendo 16:1-15

Na. 3: Kwa Nini Tumtumikie Yehova Bila Woga?

Na. 4: Mtu Anaweza Kupataje Imani? (rs uku. 93 ¶1-4)

Julai 14 Usomaji wa Biblia: Matendo 18-21 Wimbo 32

Sifa ya Usemi: Uanzie Wapi? (be uku. 251 ¶4–uku. 252 ¶3)

Na. 1: Kutayarisha Hotuba kwa Ajili ya Kutaniko (be uku. 47 ¶1–uku. 49 ¶1)

Na. 2: Matendo 20:1-16

Na. 3: Matendo Yanathibitisha Kwamba Mtu Ana Imani Katika Ulimwengu Mpya Wenye Uadilifu (rs uku. 93 ¶6–uku. 94 ¶3)

Na. 4: Tunaweza Kujifunza Nini Kutokana na Amri Iliyo Katika Kutoka 23:19b?

Julai 21 Usomaji wa Biblia: Matendo 22-25 Wimbo 200

Sifa ya Usemi: Wakati wa Kukubali Maoni ya Wengine (be uku. 252 ¶4–uku. 253 ¶2)

Na. 1: Kutayarisha Sehemu Mbalimbali za Mkutano wa Utumishi na Hotuba Nyinginezo (be uku. 49 ¶2–uku. 51 ¶1)

Na. 2: Matendo 22:1-16

Na. 3: Ni Katika Njia Gani Mashahidi wa Yehova Hutimiza Andiko la Yohana 13:34, 35?

Na. 4: Manabii wa Uwongo Wanaweza Kutambuliwaje? (rs uku. 176-177 ¶5)

Julai 28 Usomaji wa Biblia: Matendo 26-28 Wimbo 29

Sifa ya Usemi: Kuuliza Maswali na Kutoa Sababu (be uku. 253 ¶3–uku. 254 ¶2)

Na. 1: Matendo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 204-205 ¶32-40)

Na. 2: Matendo 26:1-18

Na. 3: Nyakati Nyingine Manabii wa Kweli Hawakufahamu Mambo Yaliyotabiriwa Yangetukia Wakati Gani au Jinsi Gani (rs uku. 177 ¶6-uku. 178 ¶3)

Na. 4: Kwa Nini Yehova Huonyesha Subira?

Ago. 4 Usomaji wa Biblia: Waroma 1-4 Wimbo 170

Sifa ya Usemi: Sababu Zenye Kusadikisha Zinazotegemea Kabisa Neno la Mungu (be uku. 255 ¶1–uku. 256 ¶2)

Na. 1: Utangulizi wa Waroma (si uku. 205-206 ¶1-7)

Na. 2: Waroma 3:1-20

Na. 3: Jinsi Ambavyo Malaika Huwalinda na Kuwaimarisha Watumishi wa Mungu

Na. 4: Mashahidi wa Yehova Huunga Mkono Ibada ya Kweli (rs uku. 178 ¶4-5)

Ago. 11 Usomaji wa Biblia: Waroma 5-8 Wimbo 207

Sifa ya Usemi: Sababu Ziwe na Uthibitisho (be uku. 256 ¶3-5)

Na. 1: Kutayarisha Hotuba za Watu Wote (be uku. 52 ¶1–uku. 54 ¶1)

Na. 2: Waroma 6:1-20

Na. 3: Mashahidi wa Yehova Hutambuliwa kwa Matunda Yao (rs uku. 179 ¶1–uku. 180 ¶2)

Na. 4: Jinsi Uadilifu Unavyoweza Kutulinda

Ago. 18 Usomaji wa Biblia: Waroma 9-12 Wimbo 152

Sifa ya Usemi: Kutoa Uthibitisho wa Kutosha (be uku. 256 ¶6–uku. 257 ¶3)

Na. 1: Waroma—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 209 ¶20-25)

Na. 2: Waroma 9:1-18

Na. 3: Hatari za Kupiga Porojo na Kueneza Uvumi

Na. 4: Kuwajibu Wale Wanaotuita Manabii wa Uwongo (rs uku. 180 ¶3-uku. 181 ¶2)

Ago. 25 Usomaji wa Biblia: Waroma 13-16 Wimbo 16

Sifa ya Usemi: Jitahidi Kugusa Moyo (be uku. 258 ¶1-5)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Sept. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 1-9 Wimbo 199

Sifa ya Usemi: Kufunua Yaliyo Katika Mioyo ya Watu (be uku. 259 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa 1 Wakorintho (si uku. 210-211 ¶1-7)

Na. 2: 1 Wakorintho 4:1-17

Na. 3: Mungu Hajamwamulia Kila Mtu Wakati wa Kufa (rs uku. 169 ¶1-3)

Na. 4: Je, Kuwa na Mali Kunathibitisha Kwamba Mtu Amebarikiwa na Mungu?

Sept. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 10-16 Wimbo 35

Sifa ya Usemi: Kuchochea Hisia Zinazofaa (be uku. 259 ¶4–uku. 260 ¶1)

Na. 1: 1 Wakorintho—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 213-214 ¶23-26)

Na. 2: 1 Wakorintho 13:1–14:6

Na. 3: Kwa Nini Watendaji wa Neno Ni Wenye Furaha?

Na. 4: Si Kila Jambo Linalotukia Ni Mapenzi ya Mungu (rs uku. 170 ¶1–uku. 171 ¶1)

Sept. 15 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 1-7 Wimbo 58

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Wamwogope Mungu (be uku. 260 ¶2-3)

Na. 1: Utangulizi wa 2 Wakorintho (si uku. 214 ¶1-4)

Na. 2: 2 Wakorintho 1:1-14

Na. 3: Mungu Hajui Wala Hapangi Mapema Kila Jambo (rs uku. 171 ¶2-4)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hushangilia Wanapoteswa?

Sept. 22 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 8-13 Wimbo 12

Sifa ya Usemi: Mungu Huchukua Mwenendo Wetu kwa Uzito (be uku. 260 ¶4–5)

Na. 1: 2 Wakorintho—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 216-217 ¶18-20)

Na. 2: 2 Wakorintho 9:1-15

Na. 3: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Si Sehemu ya Ulimwengu?

Na. 4: Uwezo wa Mungu wa Kujua na Kupanga Matukio Mapema (rs uku. 172 ¶1-4)

Sept. 29 Usomaji wa Biblia: Wagalatia 1-6 Wimbo 163

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kujichunguza (be uku. 261 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa Wagalatia na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 217-220 ¶1-6, 14-18)

Na. 2: Wagalatia 1:1-17

Na. 3: Kwa Nini Mungu Hakutumia Uwezo Wake wa Kujua Mapema Kwamba Adamu Angefanya Dhambi? (rs uku. 172 ¶5-uku. 173 ¶2)

Na. 4: Jinsi Upendo Unavyoweza Kumsaidia Mtu Aache Kuwaogopa Wanadamu

Okt. 6 Usomaji wa Biblia: Waefeso 1-6 Wimbo 99

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kutii Kutoka Moyoni (be uku. 261 ¶4-uku. 262 ¶3)

Na. 1: Utangulizi wa Waefeso na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 220-223 ¶1-8, 16-19)

Na. 2: Waefeso 3:1-19

Na. 3: Kuomba Msamaha Si Udhaifu

Na. 4: Mungu Hakupanga Mapema Mambo Ambayo Yangewapata Yakobo, Esau, na Yuda (rs uku. 173 ¶3–uku. 174 ¶1)

Okt. 13 Usomaji wa Biblia: Wafilipi 1–Wakolosai 4 Wimbo 123

Sifa ya Usemi: Kushirikiana na Yehova Ili Kugusa Mioyo ya Watu (be uku. 262 ¶4)

Na. 1: Utangulizi wa Wafilipi na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 223-225 ¶1-7, 12-14)

Na. 2: Wafilipi 3:1-16

Na. 3: Ni Katika Njia Gani Kutaniko la Kikristo Liliagizwa Kimbele? (rs uku. 174 ¶2-3)

Na. 4: a Wakolosai—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 228 ¶12-14)

Okt. 20 Usomaji wa Biblia: 1 Wathesalonike 1–2 Wathesalonike 3 Wimbo 161

Sifa ya Usemi: Kutunza Wakati (be uku. 263 ¶1–uku. 264 ¶4)

Na. 1: Utangulizi wa 1 Wathesalonike na 2 Wathesalonike na Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 229-231 ¶1-5, 13-15; uku. 232-233 ¶1-4, 10-11)

Na. 2: 1 Wathesalonike 1:1–2:8

Na. 3: Maandiko Yana Maoni Gani Kuhusu Unajimu? (rs uku. 175 ¶1–5)

Na. 4: b 1 Timotheo na 2 Timotheo—Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 236-237 ¶15-19; uku. 238-239 ¶10-12)

Okt. 27 Usomaji wa Biblia: 1 Timotheo 1–2 Timotheo 4 Wimbo 69

Sifa ya Usemi: Kutoa Himizo Linalofaa (be uku. 265 ¶1-uku. 266 ¶1)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Nov. 3 Usomaji wa Biblia: Tito 1–Filemoni Wimbo 149

Sifa ya Usemi: Kuhimiza Juu ya Msingi wa Upendo (be uku. 266 ¶2-5)

Na. 1: Utangulizi wa Tito na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 239-241 ¶1-4, 8-10)

Na. 2: Tito 1:1-16

Na. 3: Kuna Sababu Gani Nzuri za Kuamini Kwamba Kuna Mungu? (rs uku. 215-216 ¶3)

Na. 4: c Filemoni—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 242-243 ¶7-10)

Nov. 10 Usomaji wa Biblia: Waebrania 1-8 Wimbo 144

Sifa ya Usemi: Kuhimiza kwa Msingi wa Maandiko (be uku. 267 ¶1-2)

Na. 1: Utangulizi wa Waebrania (si uku. 243-244 ¶1-9)

Na. 2: Waebrania 3:1-19

Na. 3: Kuwako kwa Uovu na Kuteseka Hakuthibitishi Kwamba Hakuna Mungu (rs uku. 216 ¶4–6)

Na. 4: Tofauti Kati ya Unyenyekevu wa Kweli na Unyenyekevu wa Uwongo

Nov. 17 Usomaji wa Biblia: Waebrania 9-13 Wimbo 28

Sifa ya Usemi: Kuwa na Uhuru wa Kusema (be uku. 267 ¶3-4)

Na. 1: Waebrania—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 247 ¶23-27)

Na. 2: Waebrania 10:1-17

Na. 3: Mungu Ni Mtu Halisi Aliye na Hisia (rs uku. 217 ¶1–7)

Na. 4: Jinsi Msamaha Unavyoendeleza Umoja

Nov. 24 Usomaji wa Biblia: Yakobo 1-5 Wimbo 88

Sifa ya Usemi: Kwa Nini Ni Muhimu Kuwa Mwenye Kutia Moyo? (be uku. 268 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa Yakobo na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 248-250 ¶1-7, 15-17)

Na. 2: Yakobo 1:1-21

Na. 3: Mungu Hana Mwanzo (rs uku. 217 ¶8-uku. 218 ¶3)

Na. 4: Jinsi Ambavyo “Rehema Hufurahi kwa Njia ya Ushindi Juu ya Hukumu” (Yak. 2:13)

Des. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Petro 1–2 Petro 3 Wimbo 18

Sifa ya Usemi: Kukumbuka Matendo ya Yehova (be uku. 268 ¶4–uku. 269 ¶2)

Na. 1: Utangulizi wa 1 Petro na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 251-253 ¶1-5, 11-13)

Na. 2: 1 Petro 2:1-17

Na. 3: Kulitumia Jina la Mungu Ni Muhimu Ili Kupata Wokovu (rs uku. 218 ¶4-uku. 219 ¶3)

Na. 4: d 2 Petro—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 255 ¶8-10)

Des. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Yohana 1–Yuda Wimbo 50

Sifa ya Usemi: Kuonyesha Jinsi Ambavyo Yehova Amewasaidia Watu Wake (be uku. 269 ¶3-5)

Na. 1: Utangulizi wa 1 Yohana, 2 Yohana, na 3 Yohana na Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 256-258 ¶1-5, 11-13; uku. 259 ¶1-3, 5; uku. 260-261 ¶1-3, 5)

Na. 2: 1 Yohana 4:1-16

Na. 3: Je, Dini Zote Ni Nzuri? (rs uku. 219 ¶4-7)

Na. 4: e Yuda—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 262-263 ¶8-10)

Des. 15 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 1-6 Wimbo 219

Sifa ya Usemi: Furahia Matendo ya Mungu Sasa (be uku. 270 ¶1–uku. 271 ¶2)

Na. 1: Utangulizi wa Ufunuo (si uku. 263-264 ¶1-6)

Na. 2: Ufunuo 3:1-13

Na. 3: Yesu Ni “Mungu” wa Aina Gani? (rs uku. 219 ¶8-9)

Na. 4: Subira na Rehema Zina Mipaka

Des. 22 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 7-14 Wimbo 21

Sifa ya Usemi: Faidika Kabisa na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (be uku. 5 ¶1–uku. 8 ¶1)

Na. 1: Ufunuo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 268-269 ¶28-34)

Na. 2: Ufunuo 8:1-13

Na. 3: Kujibu Maswali ya Watu Wasiomwamini Mungu (rs uku. 220 ¶1–uku. 221 ¶2)

Na. 4: Maneno “Mungu Ni Mkuu Kuliko Mioyo Yetu” Yanamaanisha Nini? (1 Yoh. 3:20)

Des. 29 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 15-22 Wimbo 60

Sifa ya Usemi: Kusoma kwa Usahihi (be uku. 83 ¶1-5)

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

[Maelezo ya Chini]

a Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.

b Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.

c Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.

d Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.

e Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki