Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/07 uku. 1
  • Tembeeni Kama Watu Wenye Hekima

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tembeeni Kama Watu Wenye Hekima
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Shiriki Kikamili Katika Mavuno Makubwa ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Tunafurahia Kutumiwa Kabisa Katika Utumishi wa Yehova!
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 11/07 uku. 1

Tembeeni Kama Watu Wenye Hekima

1 Yesu alipowaomba wavuvi wanne wawe wafuasi wake, hawakukawia kufanya uamuzi bali ‘mara moja walimfuata.’ (Mt. 4:18-22) Sauli wa Tarso alipogeuza imani yake na akaanza kuona tena, yeye pia hakukawia bali ‘alianza mara moja kumhubiri Yesu katika masinagogi.’ (Mdo. 9:20) Wakati husonga daima; na ukishapita, hauwezi kurudishwa nyuma. Kwa sababu hiyo, ni muhimu ‘tutembee kama watu wenye hekima’ kuhusu jinsi tunavyotumia wakati wetu.—Efe. 5:15, 16.

2 Tukio Lisilotazamiwa: Huenda nafasi tuliyo nayo leo ya kumtumikia Yehova isiwepo kesho. (Yak. 4:14) Hakuna mtu anayeweza kuepuka “tukio lisilotazamiwa.” (Mhu. 9:11) Isitoshe, sote tunazeeka, na “siku zenye msiba” ambazo huja na uzee, na ambazo hutuzuia kutimiza mengi katika utumishi wa Yehova haziepukiki katika mfumo huu wa mambo. (Mhu. 12:1) Kwa hiyo, si jambo la hekima kukawia kujiweka wakfu kwa Mungu au kungojea hadi kuwe na hali zinazofaa ili kupanua utumishi wetu kadiri tuwezavyo kwa sasa. (Luka 9:59-62) Abrahamu alikuwa na amani miaka yake ya baadaye, naye alikufa akiwa “mzee na mwenye kutosheka” kwa sababu alitumia maisha yake kwa hekima, akijitoa kabisa kwa Yehova.—Mwa. 25:8.

3 Wakati Umepungua: Pia, tunataka kutumia wakati wetu kwa hekima kwa sababu “wakati uliobaki umepungua.” (1 Kor. 7:29-31) Hivi karibuni, mfumo huu wa kale utakwisha. Fursa za kushiriki katika ukusanyaji mkubwa wa watu wenye mfano wa kondoo wakati wa “mavuno ya dunia” zitakwisha. (Ufu. 14:15) Tunahitaji kuwa waangalifu ili tusiruhusu mahangaiko ya maisha na mambo yanayokengeusha fikira yachukue wakati ambao tungetumia vizuri katika huduma. (Luka 21:34, 35) Itafurahisha kama nini kutafakari yaliyopita tukijua kwamba tulishiriki kikamili katika kazi ya uvunaji!

4 Lazima tuwe waangalifu daima ili tusikose mapendeleo yenye kuleta shangwe ambayo huenda tukapata. Na tuazimie kumtumikia Yehova kadiri tunavyoweza “maadamu inaweza kuitwa ‘Leo.’” (Ebr. 3:13) Kwa kufanya hivyo, tutaonyesha kwamba kweli tuna hekima, kwa sababu “yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yoh. 2:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki