Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/07 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 12
  • Juma Linaloanza Novemba 19
  • Juma Linaloanza Novemba 26
  • Juma Linaloanza Desemba 3
Huduma ya Ufalme—2007
km 11/07 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Novemba 12

Wimbo 59

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na Amkeni! la Oktoba. Katika kila onyesho magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa.

Dak. 15: “Fedha Ni Yangu, na Dhahabu Ni Yangu.” Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2007, ukurasa wa 17 kama wacho ni “Fedha Ni Yangu, na Dhahabu Ni Yangu.” Ikiwa gazeti hilo halipatikani, tumia makala yenye kichwa “Kujenga kwa Umoja Ili Kumsifu Mungu” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2006, ukurasa wa 17-21.

Dak. 20: “Tembeeni Kama Watu Wenye Hekima.”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 192.

Juma Linaloanza Novemba 19

Wimbo 109

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Taja toleo la mwezi wa Desemba, na upange kuwe na onyesho moja la jinsi ya kulitoa.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Usiwanyime Watu Mema!”b Unapochunguza fungu la 5, tia ndani maelezo kutoka kwa ndugu au dada ambao wamejifunza na watu fulani, nao wakawa Mashahidi. Kuongoza funzo la Biblia linalofanya maendeleo kunaridhisha na kufurahisha jinsi gani? Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo.

Wimbo 96.

Juma Linaloanza Novemba 26

Wimbo 172

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba.

Dak. 15: Je, Unaweza Kupanuka Katika Upendo? Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2007, ukurasa wa 9-11.

Dak. 20: Vijana—Mnawezaje Kumsifu Yehova? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2005, ukurasa wa 26-28, mafungu ya 15-19. Tumia maswali yaliyo katika makala hiyo. Unapozungumzia fungu la 18, waombe vijana waeleze jinsi wamewahubiria wanafunzi au walimu shuleni.

Wimbo 5.

Juma Linaloanza Desemba 3

Wimbo 77

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Pitia Sanduku la Swali.

Dak. 15: Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 2006, ukurasa wa 10-13. Tia ndani mahojiano mafupi ya wazee au watumishi wa huduma wowote ambao wamehudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma. Shule hiyo imewasaidiaje wafanye maendeleo wakiwa wahubiri, wachungaji, na walimu? Watie moyo akina ndugu wanaostahili waweke mradi wa kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma.

Dak. 15: “Tunawaambia Wengine Kuhusu Tumaini Letu la Ufalme.”c Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 173.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki