Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 kur. 3-6
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Majira ya Ukumbusho—Fursa ya Kuongeza Utendaji!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 kur. 3-6

‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’

1. Ni habari gani njema ambazo tunapaswa kuwaambia watu?

1 Katika ulimwengu ambamo ni nadra sana kupata habari njema, sisi tuna pendeleo la “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu.” (Mdo. 20:24) Hilo linatia ndani kuwajulisha watu kwamba hivi karibuni, “siku za mwisho” zitakwisha na mahali pake patachukuliwa na ulimwengu mpya wa Yehova wenye uadilifu, ambamo ‘mambo ya zamani yatakuwa yamepitilia mbali.’ (2 Tim. 3:1-5; Ufu. 21:4) Wakati huo magonjwa hayatakuwapo tena. (Isa. 33:24) Wapendwa waliokufa watatoka katika makaburi ya ukumbusho na kuungana tena na familia na marafiki wao. (Yoh. 5:28, 29) Dunia nzima itafanywa kuwa paradiso maridadi. (Isa. 65:21-23) Hizo ni baadhi tu ya habari njema ambazo tunapaswa kuwaambia watu!

2. Kwa nini majira ya Ukumbusho ni fursa nzuri ya kuhubiri habari njema?

2 Miezi ya Machi, Aprili, na Mei itatokeza fursa nzuri ya kutangaza habari njema kama hizo. Katika nchi nyingi, miezi hiyo huwa na hali nzuri ya hewa na hilo hufanya iwezekane kushiriki katika huduma kwa muda mrefu. Isitoshe, Ukumbusho, ambalo ndilo tukio muhimu zaidi katika mwaka, utaadhimishwa ulimwenguni pote Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kutua. Huu ndio wakati wa kuanza kufanya mipango ili uweze kushiriki zaidi katika huduma ya shambani.

3. Ni nini kitakachotusaidia kuongeza utendaji wetu tukiwa familia?

3 Upainia Msaidizi: Je, unaweza kupanga ratiba yako ili uweze kufanya upainia msaidizi mwezi mmoja, miwili, au miezi yote mitatu? Mnaweza kuzungumzia jambo hilo mkiwa familia wakati wa funzo lenu la familia linalofuata. Kukiwa na ushirikiano mzuri, mtu mmoja au wawili katika familia anaweza kuwa painia msaidizi. (Met. 15:22) Sali kuhusu jambo hilo, na utaona jinsi ambavyo Yehova atabariki jitihada zako. (Met. 16:3) Hata ikiwa hakuna yeyote katika familia anayeweza kufanya upainia msaidizi, wote katika familia wanaweza kujiwekea miradi hususa ya kutumia wakati mwingi zaidi katika huduma wanapohubiri na wale ambao wanapainia.

4. Ikiwa tunafanya kazi ya wakati wote, tunaweza kupangaje ratiba yetu ili tuweze kufanya upainia msaidizi?

4 Ikiwa unafanya kazi ya wakati wote, kuwa na ratiba nzuri kunaweza kukusaidia kufanya upainia msaidizi. Huenda ukatumia muda wako wa chakula cha mchana kuhubiri. Au unaweza kuomba eneo la kibinafsi karibu na mahali unapoishi au unapofanya kazi na ulihubiri saa moja hivi kabla au baada ya kazi. Utapata muda zaidi wa kuhubiri kwa kupanga kufanya mambo yasiyo muhimu mwezi mwingine na kuhubiri siku nzima Jumamosi na Jumapili. Wengine wamechukua likizo ya siku moja au mbili ili kuhubiri.

5. Unaweza kuwasaidiaje wagonjwa au wazee kwa umri kufanya upainia msaidizi?

5 Ikiwa wewe ni mgonjwa, mzee kwa umri, au huna nguvu, unaweza kufanya upainia msaidizi kwa kuhubiri saa chache kila siku. Mwombe Yehova akupe “nguvu zinazopita zile za kawaida.” (2 Kor. 4:7) Dada mmoja mwenye umri wa miaka 106 aliweza kufanya upainia msaidizi! Akisaidiwa na watu wa ukoo ambao ni Mashahidi na wahubiri wengine katika kutaniko, alihubiri nyumba kwa nyumba, akafanya ziara za kurudia, akashiriki katika mafunzo ya Biblia, na kushiriki katika sehemu nyingine za huduma. Alisaidia kuanzisha mafunzo kumi ya Biblia. Anasema hivi: “Ninapofikiria fursa hiyo ya pekee niliyopata ya kuwa painia msaidizi, moyo wangu hufurika kwa upendo na shukrani kwa Yehova, Mwana wake, na tengenezo Lake lenye upendo. Kwa kweli ninataka kumwambia Yehova, ‘Asante sana!’”

6. Vijana waliobatizwa wanawezaje kufanya upainia msaidizi hata wakiwa shuleni?

6 Ikiwa wewe ni kijana aliyebatizwa na unaenda shuleni, unaweza pia kufanya upainia msaidizi. Kama watu wanaofanya kazi ya wakati wote, huenda ukapanga kwenda kuhubiri Jumamosi na Jumapili. Pengine unaweza pia kuhubiri saa moja au zaidi baada ya shule siku fulani. Je, kuna sikukuu yoyote unayoweza kutumia kwenda utumishini? Ikiwa ungependa kufanya upainia msaidizi, zungumzia jambo hilo pamoja na wazazi wako.

7. Wazee wanaweza kuchocheaje roho ya upainia wakati wa majira ya Ukumbusho?

7 Chochea Roho ya Upainia: Wazee wanaweza kuchochea roho ya upainia katika kutaniko kwa mfano wao. (1 Pet. 5:2, 3) Wanaweza kupanga mikutano ya utumishi wa shambani kwa ajili ya wale ambao watahubiri mapema asubuhi, baada ya shule, au baada ya kazi. Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuhakikisha kwamba kuna ndugu anayestahili ambaye ataongoza mkutano wa utumishi wa shambani, na kwamba kuna eneo na pia magazeti na vichapo vya kutosha kwa ajili ya miezi hiyo ya utendaji wa pekee.

8. Tunajifunza nini kutokana na jambo lililoonwa katika kutaniko moja?

8 Katika kutaniko moja, wazee walianza kuwatia moyo wahubiri wafanye upainia msaidizi miezi kadhaa kabla ya majira ya Ukumbusho. Kila juma walitangaza majina ya wahubiri ambao wamechukua upainia msaidizi. Kwa kufanya hivyo, wale waliotaka kuongeza utumishi wao walikuwa na uhakika kwamba watapata watu wa kuhubiri nao. Mikutano ya ziada kwa ajili ya utumishi wa shambani ilipangwa mapema asubuhi na jioni. Matokeo yakawa kwamba wahubiri 53, yaani, karibu nusu ya wahubiri katika kutaniko hilo walifanya upainia msaidizi mwezi wa Aprili!

9. Kwa nini majira ya Ukumbusho ni wakati mzuri kwa wale wanaostahili kuanza kuhubiri habari njema?

9 Wasaidie Wengine Wahubiri: Wapya na vijana wanapostahili kuwa wahubiri, wanaweza kuhubiri pamoja na wahubiri wenye uzoefu. Fursa hiyo inaweza kujitokeza katika majira ya Ukumbusho wakati wengi katika kutaniko watakuwa wakiongeza utendaji wao. Je, una mwanafunzi wa Biblia ambaye anafanya maendeleo na anaishi kupatana na viwango vya Yehova vya uadilifu? Je, una watoto wenye tabia nzuri ambao wanafanya maendeleo mazuri lakini wao bado si wahubiri? Ikiwa mwanafunzi wa Biblia au mtoto wako anataka kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa na unahisi kwamba anastahili, mjulishe mmoja wa wazee. Mwangalizi-msimamizi atapanga wazee wawili wazungumze nawe pamoja na mtoto au mwanafunzi wako kuhusu jambo hilo.

10. Wazee wanaweza kufanya nini ili kuwasaidia wale wasiotenda?

10 Miezi inayokuja itakuwa wakati mzuri pia kwa wale ambao wamekuwa wasiotenda kuanza tena kuhubiri pamoja na kutaniko. Waangalizi wa Mafunzo ya Vitabu ya Kutaniko wanapaswa kujitahidi sana kuwatembelea na kuwaalika wale wasiotenda washiriki pamoja nao katika huduma. Ikiwa mhubiri amekuwa asiyetenda kwa muda mrefu, wazee wawili wanapaswa kuzungumza naye kwanza ili kuona kama anastahili kuhubiri.—km 11/00 uku. 3.

11. Ni nini wonyesho mkubwa zaidi wa “fadhili zisizostahiliwa za Mungu?”

11 Jitayarishe kwa Ajili ya Ukumbusho: Ukumbusho ndio wonyesho mkubwa zaidi wa “fadhili zisizostahiliwa za Mungu.” (Mdo. 20:24) Ulimwenguni pote, mamilioni ya watu wenye uthamini watakusanyika pamoja Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kutua ili kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Tunataka kuwaalika na kuwasaidia wote wenye mioyo minyoofu wahudhurie tukio hili muhimu ambalo linaonyesha wazi fadhili zisizostahiliwa za Yehova kwa wanadamu.

12. Tutawaalika nani kwenye Ukumbusho?

12 Andika orodha ya watu ambao ungependa kualika. Bila shaka orodha yako itatia ndani watu wa ukoo, majirani, wafanyakazi na wanashule wenzako, wanafunzi wako wa Biblia wa sasa na wa zamani, na wengine wote ambao wewe huwatembelea kwa kawaida. Ikiwa baadhi ya watu unaoalika wana maswali kuhusu Ukumbusho, unaweza kutumia nyongeza kuhusu Mlo wa Jioni wa Bwana iliyo kwenye ukurasa wa 206-208 wa kitabu Biblia Inafundisha. Hilo linaweza hata kufungua njia ya kuanzisha funzo la Biblia kwa kuwa utapata fursa ya kumwonyesha kitabu ambacho tunatumia kuongoza mafunzo ya Biblia.

13. Yehova alibarikije jitihada za wahubiri wawili za kuwaalika wengine kwenye Ukumbusho?

13 Dada mmoja aliandika majina ya familia 48 ambazo alipanga kualika. Mara tu alipoalika familia moja, alitia alama kwenye orodha yake na akaandika tarehe ambayo aliwapa mwaliko. Alifurahi sana watu 26 alioalika walipokuja kwenye Ukumbusho! Ndugu ambaye ana duka alimwalika mfanyakazi wake ambaye zamani alikuwa kasisi. Mtu huyo alihudhuria na baadaye alisema, “Nilijifunza mengi kuhusu Biblia katika muda wa saa moja kuliko yale niliyokuwa nimejifunza kwa muda wa miaka 30 nikiwa mfuasi wa Kanisa Katoliki.” Muda mfupi baada ya Ukumbusho, mtu huyo alikubali kujifunza Biblia kupitia kitabu Biblia Inafundisha.

14. Ni kampeni gani ya ulimwenguni pote itakayoanza Machi 1?

14 Kampeni: Kuanzia Jumamosi, Machi 1 hadi Machi 22, mialiko ya pekee ya Ukumbusho itagawanywa ulimwenguni pote. Wahubiri wote watajitahidi wawezavyo kushiriki katika kampeni hiyo muhimu. Ni afadhali kumpa mwenye nyumba mwaliko huo moja kwa moja badala ya kuuacha mlangoni. Hata hivyo, ikiwa mna eneo kubwa, huenda wazee wakaamua kwamba mialiko iachwe kwenye nyumba ambazo watu hawapatikani. Jumamosi na Jumapili tutatoa magazeti ya karibuni pamoja na mwaliko huo.

15. Tunaweza kusema nini tunapompa mtu mwaliko wa Ukumbusho?

15 Kwa kuwa tuna muda mfupi wa kugawanya mialiko hiyo, ingefaa tuwe na utangulizi mfupi. Uwe mwenye urafiki na mchangamfu. Unaweza kusema hivi: “Ningependa kukualika wewe, familia yako, na marafiki wako kwenye tukio muhimu litakalofanyika Machi 22. Huu ni mwaliko wako. Habari kuhusu tukio hilo zimeonyeshwa katika mwaliko huu.” Huenda mwenye nyumba akawa na maswali. Au huenda akakubali mwaliko huo na hata kusema kwamba atafika. Andika majina ya wale wanaopendezwa kwa kadiri fulani na upange kuwarudia.

16. Ni jambo gani lililoonwa linaloonyesha umuhimu wa kampeni ya kuwaalika watu katika eneo kwenye Ukumbusho?

16 Mwaka jana, askari-jeshi mmoja alipata mwaliko wa Ukumbusho mlangoni. Aliamua kuhudhuria lakini kwanza ilibidi amwombe msimamizi wake ruhusa. Alipomwonyesha mwaliko huo, msimamizi huyo alinyamaza, kisha akamwambia kwamba wazazi wake ni Mashahidi na wakati mmoja alikuwa akihudhuria mikutano pamoja nao. Msimamizi alimpa askari-jeshi huyo ruhusa na hata akaandamana naye kwenye Ukumbusho.

17. Tunaonyeshaje kwamba hatujakosa kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu?

17 Onyesha Uthamini: Majira ya Ukumbusho ya 2008 yanapokaribia, sote na tutafakari kuhusu fadhili zisizostahiliwa ambazo Yehova ametuonyesha. Mtume Paulo aliandika hivi: “Tunawasihi ninyi pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake.” (2 Kor. 6:1) Tunaonyeshaje kwamba hatujakosa kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu? Paulo aliandika: “Bali katika kila njia tunajipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu.” (2 Kor. 6:4) Kwa hiyo, tunaonyesha uthamini wetu kwa ajili ya zawadi ambayo Yehova ametupa kupitia mwenendo wetu mzuri na kwa kuhubiri habari njema kwa bidii. Majira haya ya Ukumbusho yatatupa fursa nzuri ya kuongeza utendaji wetu, na kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Ni Nani Wanaoweza Kufanya Upainia Msaidizi?

◼ Familia

◼ Wanaofanya kazi ya wakati wote

◼ Wazee na wagonjwa

◼ Walio shuleni

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Unapotoa Mwaliko wa Ukumbusho:

◼ Zungumza kwa ufupi; uwe mchangamfu

◼ Andika majina ya wanaopendezwa na uwarudie

◼ Toa magazeti Jumamosi na Jumapili

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki