Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Desemba 15 na Amkeni! la Desemba.
Dak. 15: “Tumia Wakati Vizuri Unapokuwa Shambani.”a Hoji ndugu ambaye huongoza mkutano wa utumishi wa shambani kwa njia nzuri. Ni matayarisho gani ambayo yeye hufanya ili kuongoza mkutano huo na kutumia wakati vizuri shambani?
Dak. 20: ‘Maneno Yenu na Yawe . . . Sikuzote Yenye Kukolezwa Chumvi.’b Unaposhughulikia fungu la 2, soma Yohana 4:7-15, 39.
Juma Linaloanza Januari 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja toleo la mwezi wa Februari, na upange kuwe na onyesho moja la jinsi ya kulitoa. Ikiwa video Transfusion-Alternative Health Care—Meeting Patient Needs and Rights inapatikana, watie moyo wote waitazame ili wawe tayari itakapozungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi juma linaloanza Februari 4. Mahali ambapo video hiyo haipatikani, makala “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2004 na Oktoba 15, 2000 au makala “Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1990 itazungumziwa. Wahubiri wanaweza kupitia habari hiyo kabla ya Mkutano wa Utumishi wa juma linaloanza Februari 4.
Dak. 10: Je, Unatumia kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008 au dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2007, ikiwa kijitabu cha 2008 hakijafika kutanikoni. Zungumzia umuhimu wa kutenga dakika chache kila siku ili kusoma andiko la siku na maelezo yake. Waombe akina ndugu waeleze kuhusu mipango yao ya kusoma andiko la siku na jinsi ambavyo wamefaidika. Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo. Zungumzia kifupi andiko la mwaka la 2008.
Dak. 25: ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema.’c (Fu. 1-10) Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Mhoji mhubiri mmoja au wawili ambao walifanya upainia msaidizi mwaka uliopita licha ya ugonjwa au kuwa na shughuli nyingi. Walifauluje kufanya upainia? Walipata shangwe gani? Unapozungumzia fungu la 7, taja ratiba ya mikutano ya utumishi wa shambani kwa miezi ya Machi, Aprili, na Mei.
Juma Linaloanza Januari 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za mwezi wa Januari. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari. Baada ya kutaja kwa ufupi yaliyomo katika kila toleo, waulize wasikilizaji ni makala zipi zitakazowavutia watu katika eneo na kwa nini. Waombe wasikilizaji waeleze mambo hususa katika makala hizo ambayo wamepanga kutumia shambani. Wanaweza kuuliza maswali gani ili kuanzisha mazungumzo? Kisha wanaweza kusoma andiko gani katika makala? Watahusianishaje andiko hilo na makala? Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa magazeti hayo.
Dak. 20: ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema.’d (Fu. 11-17) Ikiwa mialiko ya pekee ya Ukumbusho imefika kutanikoni, mpe kila mtu aliyehudhuria nakala unapozungumzia fungu la 14. Taja mipango ya kutaniko lenu ya kugawa mialiko hiyo katika eneo lenu.
Dak. 15: “Wasaidie Wanafunzi wa Biblia Wawe Wahubiri wa Habari Njema ya Ufalme.”e Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.
Juma Linaloanza Februari 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia Sanduku la Swali.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 25: “Je, Unaahirisha?” Ishughulikiwe na mzee. Anza moja kwa moja mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu video Patient Needs and Rights ukitumia maswali yaliyo kwenye makala hiyo. Kwa kumalizia, soma fungu la mwisho na uwatie moyo wote wapitie kwa uangalifu makala za Mnara wa Mlinzi na Huduma Yetu ya Ufalme zilizotajwa. Mahali ambapo video hiyo haipatikani, zungumzia makala “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2004 na Oktoba 15, 2000 au makala “Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1990. Eleza jinsi ambavyo wahubiri ambao hawajajaza kadi ya DPA (Hati ya Mamlaka ya Kudumu ya Uwakilishi), ikiwa inatumika katika eneo lenu, wanaweza kutumia daftari iliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2006 kuamua visehemu vya damu na matibabu watakayokubali na kisha kuandika maamuzi yao katika kadi hiyo. Wale ambao tayari wamejaza kadi ya DPA au AMD (Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia) wanaweza kupitia tena yaliyomo, na ikiwa watabadili chochote, wajaze kadi mpya.
[Maelezo ya chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.