Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Novemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani maelezo ya mwangalizi wa utumishi juu ya jinsi kazi ya kugawa trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? inavyoendelea katika eneo lenu. Kwa kuwa wahubiri wengi wamekuwa wakitoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1 na Amkeni! la Oktoba, waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametoa magazeti hayo kwa mafanikio.
Dak. 15: Sitawisha Roho ya Upendo na Ukarimu. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 2008, ukurasa wa 6-7. Iwapo toleo hili la Mnara wa Mlinzi halipatikani, tumia toleo la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2007, ukurasa wa 17-21.
Dak. 20: “Tuna Hazina za Kuwagawia Wengine.”a Unapozungumzia fungu la 2, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu kweli za Biblia ambazo ziliwavutia kujiunga na tengenezo la Yehova, au kuhusu kweli ambazo wamethamini zaidi tangu wabatizwe.
Juma Linaloanza Novemba 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: Sanduku la Swali.b
Dak. 20: “Unaweza Kufundisha!”c Mhoji mhubiri au painia ambaye wakati mmoja alihisi kwamba hawezi kuongoza funzo la Biblia. Alimtegemeaje Yehova ili apate msaada? Tengenezo limemsaidia kwa njia gani hususa kupata ustadi wa kuongoza funzo la Biblia? Amepata thawabu gani kwa kuongoza mafunzo ya Biblia?
Juma Linaloanza Novemba 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Taja toleo la mwezi wa Desemba, na upange kuwe na onyesho moja au mawili.
Dak. 20: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 15: Kujitayarisha Kutoa Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba. Pitia magazeti hayo kwa ufupi, kisha uwaulize wasikilizaji ni makala gani ambazo huenda zikawavutia watu zaidi katika eneo lenu. Ni maswali na maandiko gani unayoweza kutumia unapomwonyesha mtu makala hizo? Panga kuwe na onyesho la jinsi mojawapo ya mapendekezo katika Huduma Yetu ya Ufalme linavyoweza kutumiwa. Pia, panga mmoja wa wazee atayarishe onyesho fupi akitumia makala inayofaa eneo lenu.
Juma Linaloanza Desemba 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za mwezi wa Novemba.
Dak. 15: Mambo yaliyoonwa ya kwenu. Lieleze kutaniko ni kwa kadiri gani eneo lilihubiriwa wakati wa kugawa trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? Waombe wasikilizaji waeleze mambo mazuri yaliyoonwa walipokuwa wakigawa trakti hiyo, au kuitumia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pia, eleza mambo yenye kutia moyo yaliyoonwa wakati wa kutoa kitabu Biblia Inafundisha mwezi wa Novemba. Jambo moja au mawili yenye kupendeza yanaweza kuigizwa.
Dak. 20: “Watayarishe Wapya Wakabili Upinzani.”d Unapozungumzia fungu la 2, taja kwa ufupi jinsi habari katika kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa “Mashahidi wa Yehova” inavyoweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia kujibu maswali ya watu wa ukoo na marafiki wanaohangaika kuwahusu.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.