Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 23
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 23
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
lv sura ya 1 ¶1-9, utangulizi
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mwanzo 32-35
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo. Taja toleo la mwezi wa Machi.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari. Baada ya kutaja kifupi mambo yaliyo katika magazeti hayo, waombe wasikilizaji wataje makala zinazoweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini. Waombe wasikilizaji wataje swali wanaloweza kutumia ili kuanzisha mazungumzo, kisha wataje andiko ambalo wanaweza kusoma kabla ya kutoa magazeti hayo. Malizia kwa kuonyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Mzee anaweza kuzungumzia jinsi tunavyopaswa kuwaona wale ambao wametengwa au wamejitenga na ushirika akitumia nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2002.
Dak. 10: Je, Unatumia Kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea utangulizi wa kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2009. Zungumzia umuhimu wa kutenga dakika chache kila siku ili kusoma Andiko la siku na maelezo yake. Waombe wasikilizaji waeleze kuhusu mipango yao ya kuzungumzia andiko la siku na jinsi ambavyo wamefaidika. Ikiwa kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2009 hakijafika kutanikoni, tumia utangulizi wa kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008.