Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa wenye nyumba tayari wana kitabu hicho, wahubiri wanaweza kutoa kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Julai na Agosti: Wahubiri wanaweza kutoa yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zinazopatikana: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, au broshua nyingine yoyote ya lugha ya kienyeji inayopatikana. Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Inapowezekana, wahubiri watajitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza mtu anapochukua kitabu. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi kitabu hicho kinavyoweza kumnufaisha kwa kumwonyesha kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa.
◼ Jitihada nyingi zitafanywa ili kutangaza makusanyiko ya wilaya na ya kimataifa ya mwaka wa 2009 yatakayofanywa duniani kote. Wahubiri watakuwa na pendeleo la kugawa mwaliko wa pekee katika eneo lao. Kampeni ya kugawa mwaliko huo inapaswa kufanywa majuma matatu kabla ya kusanyiko ambalo kutaniko litahudhuria.
◼ Wahubiri wote watapata beji za kusanyiko kupitia kutaniko. Ndugu kutoka nchi nyingine watakaohudhuria kusanyiko la kimataifa watatumia beji ileile.
◼ Huenda ratiba za mikutano zikabadilishwa ikihitajika ili ndugu waweze kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Endeleeni Kukesha!” Katika Mkutano wa Utumishi wa mwisho kabla ya kuhudhuria kusanyiko, mashauri na vikumbusho vinavyofaa katika eneo lenu vinapaswa kupitiwa. Mwezi mmoja au miwili baada ya kusanyiko lenu, sehemu ya mahitaji ya kwenu inaweza kutumiwa ili kupitia mambo makuu ya kusanyiko ambayo wahubiri wameona kuwa yenye manufaa katika huduma.