Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Julai na Agosti: Wahubiri wanaweza kutoa yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zinazopatikana: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, au broshua nyingine yoyote ya lugha ya kienyeji inayopatikana. Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Inapowezekana, wahubiri watajitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza mtu anapochukua kitabu. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi kitabu hicho kinavyoweza kumnufaisha kwa kumwonyesha kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana trakti hiyo, mhubiri anapaswa kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Agosti una miisho-juma mitano, ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Iwapo unapanga kutembelea nchi ambayo haijaorodheshwa katika ripoti ya utumishi ya mwaka huu au anwani yake haijaonyeshwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni zaidi, tafadhali wasiliana na ofisi yenu ya tawi ili ujue hatua za tahadhari unazopaswa kuchukua au maagizo hususa unayohitaji kufuata. Huenda ikawa kazi ya Ufalme katika eneo hilo imewekewa vizuizi. (Mt. 10:16) Katika nchi fulani huenda lisiwe jambo la busara kwa wageni kuwasiliana na Mashahidi wenyeji au makutaniko. Huenda ofisi ya tawi itakupa pia mwelekezo kuhusu mahubiri yasiyo rasmi au kubeba vitabu. Ukifuata mwelekezo unaotolewa utaepuka mambo mengi yanayoweza kukuletea matatizo au kuathiri kazi ya Ufalme.—1 Kor. 14:33, 40.