Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/09 uku. 2
  • Jitolee kwa Nafsi Yote Kuwasaidia Wanafunzi Wako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitolee kwa Nafsi Yote Kuwasaidia Wanafunzi Wako
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Mkiwa Kutaniko, Wasaidieni Wanafunzi wa Biblia Wafikie Hatua ya Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 12/09 uku. 2

Jitolee kwa Nafsi Yote Kuwasaidia Wanafunzi Wako

1. Ni nini kinachohitajika ili kumsaidia mwanafunzi wa Biblia?

1 Ili kumsaidia mwanafunzi wa Biblia kuchukua hatua ya kujiweka wakfu, mengi zaidi yanahitajika kuliko kuongoza funzo la Biblia pamoja naye kwa ukawaida. Mtume Paulo alilinganisha uhusiano wake pamoja na wale aliowafundisha na jinsi mama anayenyonyesha anavyowatunza kwa upendo watoto wake. Sisi pia tunafurahi kujitolea kwa nafsi yote, au “kuwapa [wanafunzi wetu] nafsi zetu,” ili kuwasaidia wafanye maendeleo ya kiroho.—1 The. 2:7-9.

2. Kwa nini tunapaswa kuonyesha kwamba tunamjali mwanafunzi, na tunawezaje kufanya hivyo?

2 Mjali Mwanafunzi: Mwanafunzi wa Biblia anapofanya maendeleo, dhamiri yake itamsukuma aache kushirikiana na watu ambao hawaishi kupatana na kanuni za Biblia. (1 Pet. 4:4) Huenda akatengwa na familia yake. (Mt. 10:34-36) Sisi tunaweza kujaza pengo hilo kwa kuonyesha tunamjali na tunampenda. Ndugu mmoja ambaye amekuwa mmishonari kwa muda mrefu anapendekeza: “Usiwe na haraka kuondoka baada ya funzo. Iwapo inafaa, ongea naye kidogo baada ya funzo.” Uwe macho kutambua kama mwanafunzi anahitaji msaada fulani. Kwa mfano, labda unaweza kumtembelea au kumpigia simu anapokuwa mgonjwa. Au, ikifaa, labda unaweza kuketi karibu naye wakati wa mikutano ili kumsaidia kuwaangalia watoto.

3. Tunaweza kufanya nini ili kumsaidia mwanafunzi wetu apate kutiwa moyo na ndugu kutanikoni?

3 Kutaniko Linavyoweza Kusaidia: Unapohubiri karibu na mahali ambapo mwanafunzi wako anaishi, mtembelee na umjulishe kwa mhubiri mwenzako. Inapofaa, waombe wahubiri wengine, hata wazee wa kutaniko, waandamane nawe kwenye funzo. Pia, punde baada ya kuanzisha funzo, mtie moyo mwanafunzi wako wa Biblia ahudhurie mikutano kwenye Jumba la Ufalme. Anapohudhuria mikutano atakuwa na ushirika unaojenga pamoja na ndugu na dada kutanikoni, ambao hatimaye huenda wakawa familia yake ya kiroho.—Marko 10:29, 30; Ebr. 10:24, 25.

4. Huenda tukapata thawabu gani kwa sababu ya bidii yetu?

4 Mzazi ambaye anawafundisha watoto wake mambo ya kiroho bila kuchoka, anafurahi sana wanapoamua kumtumikia Yehova na kutembea katika kweli. (3 Yoh. 4) Tunaweza kupata furaha iyo hiyo tunapojitolea kwa nafsi yote kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki