Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 28
JUMA LINALOANZA DESEMBA 28
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
lv sura ya 14 ¶15-19, sanduku kwenye uku. 167
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 12-15
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo. Taja makala “Je, Uko Tayari Kumwimbia Yehova Kwenye Mikutano Yetu?” Watie wote moyo waje na kitabu chao kipya cha nyimbo kuanzia Januari.
Dak. 10: Jinsi ya Kujibu. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu. Panga onyesho fupi kuhusu jinsi ya kujibu kipingamizi kimoja cha kawaida. (Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 38-42.)
Dak. 10: Kuanzisha Mafunzo ya Biblia. Tangaza tarehe ya siku inayofuata ambayo imetengwa kwa kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Wahubiri wa kutaniko lenu wamepata matokeo gani wakati wa kuwatolea watu mafunzo ya Biblia? Mwombe painia au mhubiri aeleze au aonyeshe njia ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ambayo imefanikiwa katika eneo lenu
Dak. 10: Toleo la Januari. Pitia kifupi toleo la Januari. Zungumza pamoja na mhubiri kuhusu njia za kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu hicho katika mahubiri yasiyo rasmi. Watie wote moyo wawe na lengo la kuanzisha funzo la Biblia katika mwezi wa Januari.