Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 21
JUMA LINALOANZA DESEMBA 21
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
lv sura ya 14 ¶10-14, sanduku kwenye uku. 164-165, nyongeza kwenye uku. 222-223
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 9-11
Na. 1: Yoshua 9:1-15
Na. 2: Jinsi Tunavyoweza Kujua Har-Magedoni Imekaribia (lr sura ya 47)
Na. 3: Unaweza Kuishi Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu Wenye Amani (lr sura ya 48)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Panga onyesho kuhusu mwangalizi wa kikundi anayemweleza mhubiri kijana kwa nini ameamua kutumia njia fulani ya kutoa magazeti, na ni swali na andiko gani ambalo amepanga kutumia. Kijana mhubiri naye anaeleza kwamba amefikiria kutumia njia fulani lakini angehitaji msaada wa kuiboresha. Kwa kutumia makala ambayo alikuwa amechagua, wanatunga swali na kuchagua andiko ambalo atasoma.
Dak. 15: “Jitolee kwa Nafsi Yote Kuwasaidia Wanafunzi Wako.” Mazungumzo kwa maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia fungu la 2, mhoji mhubiri kuhusu jinsi anavyojitahidi kuonyesha kwamba anawajali wanafunzi wake. Matokeo yamekuwa nini? Pia, mhoji mhubiri ambaye amenufaika kwa sababu mwalimu wake wa Biblia alimjali kikweli.