Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/09 uku. 1
  • Hubiri kwa Bidii!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hubiri kwa Bidii!
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Linda Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Jinsi ya Kusitawisha Hisi ya Uharaka Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • “Siku Kuu ya Yehova Iko Karibu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 12/09 uku. 1

Hubiri kwa Bidii!

1. Tunapaswa kutia maanani maneno gani ya Paulo leo?

1 “Lihubiri neno . . . kwa bidii.” (2 Tim. 4:2) Kwa nini maneno haya ya Paulo ni muhimu sana leo? Maneno yake yanaweza kuwa na matokeo gani katika maisha yetu na ya wengine?

2. Kwa nini tunawatafuta kwa bidii wale ambao hawajasikia habari njema?

2 Uhai Unahusika: Mamilioni ya watu duniani kote bado wanahitaji kusikia habari njema ili wapate fursa ya kuokolewa. (Rom. 10:13-15; 1 Tim. 4:16) Watu wengi wenye moyo mweupe wanapatikana katika maeneo yanayohubiriwa mara nyingi. Tukihubiri siku au saa tofauti, huenda tukampata mtu ambaye hatujamhubiria bado. Tunapojitahidi kwa bidii kumhubiria kila mtu katika eneo letu, tutakuwa na dhamiri njema na tutaepuka hatia ya damu.—Mdo. 20:26.

3. Tunaweza kutumia wakati wetu vizuri jinsi gani katika huduma?

3 Licha ya kukabili upinzani mkali, Wakristo wa karne ya kwanza ‘walijaza Yerusalemu fundisho lao.’ (Mdo. 5:28) Je, tumeazimia “kutoa ushahidi kamili” kama walivyofanya? (Mdo. 10:42) Tunapokuwa katika utumishi, je, tunatumia wakati vizuri? Iwapo tunahitaji kuwangojea wahubiri wengine kwa sababu fulani, je, tunatumia wakati huo kuongea na wapita njia?

4. Kuhubiri kwa bidii kunatusaidiaje kukesha?

4 Kuhubiri kwa Bidii Hutusaidia Kukaa Macho: Mwisho wa ulimwengu huu unapokaribia, ni lazima tukae macho na kuendelea kukesha. (1 The. 5:1-6) Tunapohubiri kwa ukawaida kuhusu tumaini letu la Ufalme, tunaepuka kulemewa na ulimwengu huu. (Luka 21:34-36) Na tukiendelea kuweka siku ya Yehova “karibu akilini,” tunasukumwa kufanya zaidi katika kazi ya kuhubiri inayookoa uhai.—2 Pet. 3:11, 12.

5. Kuthamini uhai kunatusukuma jinsi gani kuhubiri?

5 Tunapohubiri kwa bidii tunaonyesha kwamba tuna maoni ya Yehova kuhusu uhai. Yeye “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Pet. 3:9; Eze. 33:11) Na tuazimie kumsifu Yehova kwa kuwahubiria watu wengi iwezekanavyo katika eneo letu!—Zab. 109:30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki