KICHWA CHA MWEZI HUU: “Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii.”—2 Tim. 4:2.
Jinsi ya Kusitawisha Hisi ya Uharaka Katika Kazi ya Kuhubiri
Tunapaswa kusitawisha hisi ya uharaka, na ni lazima tuwe nayo ili tuokoke mwisho wa mfumo huu wa mambo. Tunaweza kuimarisha hisi yetu ya uharaka kwa kufuata vikumbusho vifuatavyo.
Sali kwa ukawaida kuhusu Ufalme. —Mt. 6:10.
Linda moyo wako kwa kusoma Biblia kila siku.—Ebr. 3:12.
Tumia wakati wako kwa hekima. —Efe. 5:15, 16; Flp. 1:10.
Uwe na jicho “rahisi.” Usikengeushwe na tamaa za ulimwengu.—Mt. 6:22, 25; 2 Tim. 4:10.
Endelea kukesha kwa kutambua utimizo wa unabii wa Biblia. —Marko 13:35-37.
Kuwa na hisi ya uharaka kutatuchochea kushiriki kikamili katika kazi ya kuhubiri inayoendelea!—Yoh. 4:34, 35.