Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki, mtolee kitabu Ujuzi, Mwabudu Mungu, broshua Anataka, au kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995. Februari: Toa kimoja kati ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Wahubiri wanapaswa kuwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia wanapomwachia mtu kitabu Biblia Inafundisha au ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki nyumbani. Aprili na Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kama vile wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo linapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kuanzia Februari, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Jinsi Ufalme wa Mungu Unavyotunufaisha Leo.”