Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 22
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 22
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Waamuzi 19-21
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Toleo la Mwezi wa Machi. Wahoji wahubiri wawili, na uwaombe waeleze ni mambo gani katika toleo la mwezi wa Machi, yaani, kitabu Biblia Inafundisha, yanayowafaa watu katika eneo lenu na jinsi ambavyo wamefaulu kuanzisha mazungumzo kwa kutumia kitabu hicho. Panga kila mmoja wao afanye onyesho au aigize jambo lililoonwa akitumia kitabu hicho kuanzisha funzo la Biblia.
Dak. 10: Watu Huchochewa Kusikiliza Tunapotoa Sababu. Hotuba inayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 251 hadi ukurasa wa 253, fungu la 2.
Dak. 10: Kuwaelekeza Wanaopendezwa Kwenye Tengenezo la Yehova. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu mafungu matatu chini ya kichwa kidogo katika ukurasa wa 99 wa kitabu Tengenezo. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamewaelekeza wanaopendezwa kwenye tengenezo la Yehova. Mhoji mhubiri ambaye alinufaika kwa sababu mwalimu wake wa Biblia alifanya hivyo.