Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 28
JUMA LINALOANZA JUNI 28
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
cf sura ya 6 ¶19-25, sanduku kwenye uku. 65
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 3-6
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 3: Matangazo.
Dak. 25: “Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe.” Mazungumzo kwa maswali na majibu. Kadiri wakati unavyoruhusu, zungumzia vikumbusho vinavyofaa eneo lenu katika sehemu ya “Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya” kwenye ukurasa wa 4.
Dak. 7: Kuzoezwa Tangu Utoto Mchanga. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Timotheo alijulikana kuwa mweneza-injili stadi na mwenye bidii. (Flp. 2:20-22) Kwa kadiri fulani, bidii yake ilichangiwa na jitihada za mama na nyanya yake za kumwekea msingi mzuri wa kiroho tangu alipokuwa mtoto mchanga. (2 Tim. 1:5; 3:15) Madokezo ya Kimaandiko yafuatayo yatawasaidia wazazi wawazoeze watoto wao kuwa waeneza-injili wazuri. Kazia madokezo mawili ambayo yanawafaa. (1) Anza kuandamana na mtoto wako katika utumishi akiwa angali mchanga; mzoeze kushiriki katika utumishi kulingana na umri na uwezo wake. (Met. 22:6) (2) Weka mfano mzuri kwa kutanguliza huduma. (Flp. 1:9, 10) (3) Kazia upendo na uthamini kwa kazi ya kuhubiri wakati wa Ibada ya Familia na pia katika nyakati nyingine. (Kum. 6:6, 7) (4) Onyesha uzuri wa kazi ya kuhubiri kupitia mtazamo na maneno yako. (Flp. 3:8; 4:8; 1 Tim. 1:12) (5) Mkiwa familia, shirikini kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri, na kuifanya kuwa sehemu ya maisha yenu. (Mdo. 5:41, 42) (6) Shirikianeni na wale ambao wana bidii katika huduma. (Met. 13:20) Waombe wasikilizaji waeleze mambo hususa ambayo wazazi wao walifanya ili kuwasaidia wafanye utumishi wao uwe wenye kufurahisha na wenye matokeo.