Ratiba ya Juma Linaloanza Julai 26
JUMA LINALOANZA JULAI 26
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 15-17
Na. 1: 1 Wafalme 15:1-15
Na. 2: Ni Nani Aliyewachochea Wanadamu Watumie Uhuru Wao wa Kujiamulia Mambo Bila Kujali Amri za Mungu? (rs uku. 334 ¶3–uku. 335 ¶1)
Na. 3: Kwa Nini Vita vya Har–Magedoni Ni vya Lazima?
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Njia za Kupanua Huduma Yako—Sehemu ya 3. Hotuba inayotegemea kitabu Tengenezo, ukurasa wa 114, fungu la 2, hadi ukurasa wa 115, fungu la 4. Wahoji wahubiri walio mfano mzuri kutanikoni na ambao wamehudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma au Shule ya Gileadi kuhusu jinsi walivyofaidika na mazoezi hayo. Ikiwa hakuna mhubiri unayeweza kuhoji katika kutaniko lenu, elezea mambo yaliyoonwa ambayo yamechapishwa.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Agosti. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tumia dakika moja au mbili kueleza mambo yaliyomo katika magazeti ya karibuni mliyo nayo. Kisha chagua makala mbili au tatu, na uwaombe wasikilizaji wapendekeze maswali na maandiko ambayo wanaweza kutumia katika utangulizi wao. Panga maonyesho ya jinsi kila makala inavyoweza kutolewa.
Dak. 10: “Hekima Huonyeshwa Kuwa Yenye Uadilifu kwa Matendo Yake.” Mazungumzo kwa maswali na majibu.