Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho, basi mtolee kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995. Februari: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuanzisha funzo ukitumia kitabu Biblia Inafundisha.
◼ Kuanzia Februari, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kweli Ina Matokeo Gani Katika Maisha Yako?”