Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Katika mwezi wa Agosti 2010, makutaniko mengi yalifanya vema katika kutoa ripoti. Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 24,515. Pia kulikuwa na kilele kipya cha mapainia wa kawaida 2,557.
Tanzania: Katika mwaka wa utumishi uliopita, kulikuwa na ongezeko la asilimia 2 ya wahubiri. Pia, kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 15,091. Mafunzo ya Biblia 22,284 yaliongozwa. Watu 47,844 walihudhuria Ukumbusho. Hiyo ni zaidi ya mara 3 ya kilele cha wahubiri!
Uganda: Mwishoni mwa mwaka wa utumishi kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 5,271. Katika mwaka huo, kulikuwa na wastani wa mafunzo ya Biblia 12,780 yaliyoongozwa kila mwezi.