Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/11 uku. 8
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 1/11 uku. 8

Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

Mnara wa Mlinzi Januari 1

Soma Mwanzo 2:16, 17, kisha useme: “Watu fulani husema kwamba Mungu alijua kimbele kwamba Adamu angefanya dhambi. Wengine wanaona kwamba onyo la Mungu lingekuwa la kinafiki ikiwa tayari alijua matokeo. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inayoanzia ukurasa wa 13 inafafanua jinsi Mungu hutumia uwezo wake wa kujua mambo ya wakati ujao.”

Amkeni! Januari

“Watu fulani wanaamini kwamba imani ya kidini inategemea hisia tu wala si mambo hakika. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, imani ya kidini inapaswa kuwa na msingi. [Soma 1 Yohana 4:1.] Makala inayoanzia ukurasa wa 28 inaeleza jinsi tunavyoweza kuhakikisha kwamba imani yetu inategemezwa kabisa na mambo hakika.”

Mnara wa Mlinzi Februari 1

“Visa vya watu kutalikiana vimeenea sana leo. Unafikiri ni nini hasa kinachosababisha hali hiyo? [Mruhusu ajibu.] Ona shauri hili ambalo wenzi wengi wa ndoa wanaliona kuwa lenye faida. [Soma 1 Wakorintho 10:24.] Gazeti hili linazungumzia mambo sita ambayo waume na wake hulalamikia, na jinsi kutumia kanuni za Biblia kunavyoweza kusaidia.”

Amkeni! Februari

“Kuna ongezeko la watu wanaopendezwa na mambo yanayohusiana na uchawi, ulozi, na hekaya za majini wanyonya-damu. Je, unafikiri kwamba mtu anaweza kujihusisha na mambo ya uchawi bila kupata madhara yoyote? [Mruhusu ajibu.] Ona onyo hili ambalo Mungu aliwapa Waisraeli wa kale. [Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu uchawi.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki