Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jul. 1
“Je, unafikiri kwamba wanadamu wanaweza kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu Mweza-Yote? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Matendo 17:27.] Makala hii inaonyesha kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu anataka tuwe na uhusiano wa karibu pamoja naye.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Amkeni! Jul.
“Burudani nyingi leo zinatia ndani mambo mengi ya kuwasiliana na pepo. Je, unafikiri kuwasiliana na pepo ni hatari? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Kumbukumbu la Torati 18:10-12.] Makala hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu hatari za kuwasiliana na pepo.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Matatizo mazito ya mazingira yanawafanya watu wengi wawe na wasiwasi kuhusu wakati ujao wa dunia. Una maoni gani kuhusu hilo? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Zaburi 37:11.] Gazeti hili linakazia sababu kadhaa za Kimaandiko za kutumaini kwamba wakati ujao utakuwa mzuri.”
Amkeni! Ago.
“Watu wengi wanaamini kwamba kuongezeka kwa joto kunahatarisha uhai duniani. Unafikiri tatizo hilo litasuluhishwaje? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Isaya 11:9.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba wanadamu wataendelea kuishi duniani.”