Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Februari: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuanzisha funzo ukitumia kitabu Biblia Inafundisha.
◼ Kichwa cha hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho wa 2011 kitakuwa “Kanuni za Biblia—Je, Zinaweza Kutusaidia Kukabiliana na Matatizo ya Leo?”
◼ Isipokuwa mkutano wa utumishi wa shambani, hakuna mikutano mingine itafanywa Jumapili, Aprili 17, siku ya Ukumbusho. Makutaniko ambayo hufanya mikutano siku hiyo yanaweza kufanya mikutano hiyo siku nyingine katika juma hilo. Iwapo makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile na haiwezekani kufanya mkutano siku nyingine, mkutano huo unaweza kufutwa. Ikiwa mkutano utafutwa, familia zinatiwa moyo zifanye Funzo la Mnara wa Mlinzi wakati wa jioni ya Ibada ya Familia.