Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Unafikiri inawezekana kujua sifa za Mungu? [Mruhusu ajibu.] Nina habari fulani zenye kupendeza kuhusiana na jambo hilo.” Soma na uzungumzie jibu la swali la 2 katika ukurasa wa 16 na pia mojawapo ya maandiko yaliyotajwa. Mtolee magazeti, na upange kurudi ili mzungumzie jibu la swali la 3.
Amkeni! Februari
“Kwa kuwa Biblia ni kitabu cha zamani sana, watu fulani hufikiri kwamba si sahihi kisayansi. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi hushangaa kwamba Biblia inasema hivi. [Soma Isaya 40:22.] Makala inayoanzia ukurasa wa 22 inajibu swali, Je, sayansi inapatana na Biblia?”
Mnara wa Mlinzi Machi 1
“Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa kazi yao ya kuhubiri. Umewahi kujiuliza kwa nini sisi hufanya kazi hii? [Mruhusu ajibu.] Ona ufafanuzi huu. [Soma Mathayo 24:14.] Gazeti hili linajibu maswali kama: Habari njema ni nini? Ufalme ni nini? Na mwisho utakaokuja ni nini?”
Amkeni! Machi
“Kwa kuwa watu wengi wanapambana na magonjwa, tunawasomea watu andiko hili lenye kutia moyo. [Soma Isaya 33:24.] Maneno hayo yatakapotimia, unafikiri maisha yatakuwa tofauti jinsi gani? [Mruhusu ajibu.] Mpaka wakati ambapo Mungu ataleta badiliko hilo, kuna hatua za msingi ambazo sote tunaweza kuchukua ili kuboresha afya yetu. Gazeti hili linaeleza hatua hizo.”