Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Februari
“Watu wengi huhisi kwamba Ibilisi ndiye anayesababisha uovu ulimwenguni. Lakini wanajiuliza: ‘Ibilisi alitoka wapi? Je, aliumbwa na Mungu?’ Unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Ona hapa panavyosema.” Mwonyeshe makala inayopatikana kwenye ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na uzungumzie fungu la kwanza na andiko lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na upange kurudi tena ili uzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Tungependa kujua maoni yako kuhusu mtu ambaye anaheshimiwa sana na Wakristo, Wayahudi, na vilevile Waislamu. Mtu huyo ni Musa. Ni jambo gani huja akilini mwako unaposikia jina hilo? [Mruhusu ajibu.] Ingawa alifanya makosa, inapendeza kuona jinsi Biblia inavyomfafanua Musa. [Soma Kumbukumbu la Torati 34:10-12.] Gazeti hili linazungumzia sifa tatu nzuri alizokuwa nazo na jinsi tunavyoweza kumwiga.”
Amkeni! Februari
“Ni jambo la kawaida siku hizi kwa watu kuhamia nchi nyingine ili kutafuta maisha mazuri zaidi. Je, unafikiri kwamba siku zote wao hupata kile wanachotafuta? [Mruhusu ajibu.] Kuhamia nchi nyingine si jambo jipya. Ona mfano huu kutoka katika kitabu cha kwanza kabisa cha Biblia. [Soma Mwanzo 46:5, 6.] Gazeti hili linazungumzia maswali haya.” Mwonyeshe mwenye nyumba maswali yanayopatikana mwishoni mwa ukurasa wa 6.