Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Februari
“Watu tunaozungumza nao wana maoni tofauti-tofauti kuhusu Biblia. Wengine wanaamini kwamba ni Neno la Mungu ilhali wengine wanaiona Biblia kuwa kitabu cha kawaida tu. Wewe una maoni gani kuhusu Biblia?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa mlinzi Februari 1
“Watu wengi wangependa kuona wakati ambapo hakutakuwa na vita. Je, unafikiri kwamba inawezekana kuwa na amani ulimwenguni pote? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Maandiko yanaahidi. [Soma Zaburi 46:9.] Inapendeza kuona kwamba mambo yaliyotukia wakati na baada ya Vita vya Ulimwengu vya Kwanza yanatupatia uhakika wa kwamba Mungu atatimiza unabii huu na kumaliza vita milele. Gazeti hili linazungumzia jambo hilo.”
Amkeni Februari
“Tumewatembelea kifupi kuzungumzia jambo linalowahangaisha wengi. Inaonekana kwamba hakuna wakati wa kutosha kutimiza kila jambo. Je, unafikiri ratiba zetu zimejaa kwa sababu tuna mambo mengi ya kufanya au tunatumia muda wetu vibaya? [Mruhusu ajibu.] Wengi hawajui kwamba Biblia ina mashauri mazuri yatakayotusaidia tutumie wakati vizuri. Huu ni mfano mmoja. [Soma Wafilipi 1:10a.] Gazeti hili linatoa mbinu nne ambazo zimewasaidia watu wengi watumie wakati wao kwa hekima zaidi.”