Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Februari
“Je, unafikiri Mungu anatumia kikundi fulani cha watu waliopangwa kwa utaratibu, au anashughulika na mtu mmojammoja? [Mruhusu ajibu.] Ona yale ambayo gazeti hili linasema kuhusu watu ambao Mungu aliwapanga kwa utaratibu miaka mingi iliyopita.” Fungua ukurasa wa 26 wa toleo la Mnara wa Mlinzi la Februari 1, na uzungumzie pamoja naye habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza, na angalau usome andiko moja lililonukuliwa. Mwachie magazeti, kisha upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Katika miaka ya hivi karibuni watu wamekuwa wakizungumza sana kuhusu Har–Magedoni. Je, unafikiri kuna jambo ambalo mwanadamu anaweza kufanya ili kuzuia Har–Magedoni isitokee? [Mruhusu ajibu.] Neno Har–Magedoni linapatikana katika andiko hili. [Soma Ufunuo 16:16. Kisha umwonyeshe jalada la gazeti.] Gazeti hili linajibu maswali hayo kwa kutegemea Biblia.”
Amkeni! Februari
“Leo watu wengi hufurahia kuwasiliana kwa kutumia Intaneti. Je, unafikiri kuna hatari yoyote ya kuwasiliana kwa njia hiyo? [Mruhusu ajibu.] Biblia ina kanuni ambazo zinaweza kutusaidia ili mawasiliano yetu kupitia Intaneti yawe salama zaidi. [Fungua ukurasa wa 6-9, na uzungumzie mojawapo ya maswali yaliyoonyeshwa, kutia ndani andiko moja.] Gazeti hili litakusaidia kutambua na kuepuka hatari zinazohusianishwa na mawasiliano kupitia Intaneti.”