Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 11
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 11
Wimbo 106 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 5 ¶7-12 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mathayo 26-28 (Dak. 10)
Na. 1: Mathayo 27:24-44 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Subira ya Mungu Huongozaje Kwenye Wokovu?—2 Pet. 3:9, 15 (Dak. 5)
Na. 3: Mtu Akisema, ‘Ninyi Mnakazia Mno Unabii’—rs uku. 346 ¶4-5 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Tunajifunza Nini? Mazungumzo. Omba msikilizaji mmoja au zaidi wasome Mathayo 6:19-21 na Luka 16:13. Zungumzia jinsi masimulizi hayo yanavyoweza kutusaidia katika huduma yetu.
Dak. 20: “Je, Wewe Utafanya Upainia Msaidizi?” Maswali na majibu. Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Baada ya kuzungumzia fungu la 2, wahoji kifupi wahubiri wawili ambao wamepanga kufanya upainia msaidizi mwezi wa Machi, mmoja ambaye hufanya kazi ya wakati wote na mwingine ambaye hawezi kutimiza mengi kwa sababu ya matatizo ya kiafya. Ni mabadiliko gani ambayo wanapanga kufanya ili wawe mapainia? Panga kuwe na onyesho la wenzi wa ndoa au familia yenye watoto wakitumia muda wa jioni ya Ibada ya Familia kufanya mipango hususa ya kuongeza huduma yao. Onyesho hilo lifanywe baada ya kuzungumzia fungu la 3.
Wimbo 122 na Sala