Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 2
JUMA LINALOANZA MEI 2
Wimbo 99 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 3 ¶4-11 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ayubu 38-42 (Dak. 10)
Na. 1: Ayubu 40:1-24 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Faida za Kuwa Wapole na Wenye Subira (Dak. 5)
Na. 3: Mtu Akisema: “Je, Umemkubali Yesu Kuwa Mwokozi wa Maisha Yako?”—rs uku. 438 ¶3-4) (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Matangazo. Panga onyesho la jinsi mhubiri anavyoweza kutumia mojawapo ya mapendekezo yaliyo katika ukurasa huu kuanzisha funzo katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Mei. Watie moyo wote washiriki.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Mei. Mazungumzo. Tumia dakika moja au mbili kupitia magazeti ya karibuni. Kisha chagua makala mbili au tatu, na uwaombe wasikilizaji wapendekeze maswali na maandiko yanayoweza kutumiwa wakati wa kutoa magazeti. Panga maonyesho kuhusu jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa kwa kutumia nakala ya Huduma Yetu ya Ufalme inayozungumzia jinsi ya kutoa magazeti hayo.
Wimbo 91 na Sala