Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 25, 2011. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 20 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 7 hadi Aprili 25, 2011.
1. Ni katika maana gani ‘watu wengi wa nchi walikuwa wakijitangaza wenyewe kuwa Wayahudi’? (Esta 8:17) [w06 3/1 uku. 11 fu. 3]
2. Kwa nini Shetani aliruhusiwa kuingia mbele za Yehova? (Ayu. 1:6; 2:1) [w06 3/15 uku. 13 fu. 6; it-2-E uku. 16 fu. 4]
3. Shetani alimaanisha nini alipouliza, “Je, Ayubu amemwogopa Mungu bure”? (Ayu. 1:9) [w94 11/15 uku. 11 fu. 6]
4. Kwa nini kujua kwamba Yehova ni “mwenye hekima moyoni na mwenye nguvu katika uwezo” kunatufanya tumtumaini kabisa? (Ayu. 9:4) [w07 5/15 uku. 25 fu. 16; it-2-E uku. 1190 fu. 3]
5. Ni katika njia gani maneno ya Elifazi kwamba mtu hunywa “ukosefu wa uadilifu kama maji” yanaonyesha kufikiri kama kwa Shetani? (Ayu. 15:16) [w10 2/15 uku. 20 fu. 1-2]
6. Tunajifunza nini kutokana na kilio cha Ayubu katika Ayubu 19:2? [w94 10/1 uku. 32 fu. 1-5]
7. Ni nini kilichomsaidia Ayubu kudumisha utimilifu wake? (Ayu. 27:5) [w09 4/15 uku. 6 fu. 17]
8. Wengine wanapokuwa na uhitaji, tunaweza kumwigaje Ayubu? (Ayu. 29:12, 13) [w02 5/15 uku. 22 fu. 19; w94 9/15 uku. 24 fu. 2]
9. Ni katika njia gani shauri la Elihu lilikuwa tofauti na lile la wale marafiki wengine watatu wa Ayubu? (Ayu. 33:1, 6) [w95 2/15 uku. 29 fu. 3]
10. Kutafakari juu ya kazi za ajabu za Yehova kunapaswa kutusaidia tutambue nini? (Ayu. 37:14) [w06 3/15 uku. 16 fu. 4]