Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, mtolee trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Unapowarudia watu waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuanzisha funzo kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia kitabu Ujuzi, au broshua Anataka au Endeleeni Kukesha! Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zinazofaa katika eneo lenu. Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, Uhai—Ulitokana na Muumba? Lasting Peace and Happiness—How to Find Them, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?