Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Juni
“Kila mmoja wetu amewahi kufiwa na mtu wa familia au rafiki. Je, una tumaini la kuwaona tena watu hao waliokufa? [Mruhusu ajibu.] Ona wazo hili lenye kufariji.” Soma na uzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, na mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Wengi wetu tunapambana sana ili kupata riziki, na wengine hata hawana mahitaji ya lazima maishani. Unafikiri kuna wakati ambapo hakutakuwa na mtu yeyote maskini? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 9:18.] Gazeti hili linaonyesha chanzo cha umaskini na kile ambacho Biblia inasema kuhusu suluhisho halisi la tatizo hilo.”
Amkeni! Juni
“Ugaidi umekuwa tatizo linalowasumbua watu ulimwenguni pote. Unafikiri chanzo chake ni nini? [Mruhusu ajibu.] Maneno haya ya Biblia yanatupa tumaini. [Soma Zaburi 72:7, 14.] Gazeti hili linaeleza baadhi ya mambo yanayosababisha ugaidi na pia linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi, na wakati ambapo ugaidi utaisha.”