Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Juni
Soma Isaya 42:8 kisha useme: “Kulingana na andiko hili, Mungu ana jina. Unafikiri ni muhimu kutumia jina la Mungu? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba nakala ya Mnara wa Mlinzi ya Juni 1 na mzungumzie habari zilizo katika ukurasa wa 16, chini ya kichwa kidogo cha kwanza. Mpe magazeti na upange kurudi ili kuzungumzia swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Ningependa kujua maoni yako kuhusiana na jambo fulani muhimu. [Fungua ukurasa wa 3, na umwonyeshe orodha.] Ni maelezo gani yanayolingana na maoni yako kuelekea Biblia? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho andiko hili linasema kuhusu Maandiko yote kwa ujumla. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linazungumzia sababu tano zinazofanya Biblia iwe kitabu cha kipekee na pia jinsi inavyoweza kutunufaisha.”
Amkeni! Juni
“Kila mwaka, mamilioni ya watu huwa wagonjwa kwa sababu ya kula chakula kinachoweza kudhuru. Je, unafikiri chakula katika eneo letu ni salama? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza njia nne za kulinda familia zetu kutokana na magonjwa yanayosababishwa na chakula. Pia, linazungumzia ahadi ya Biblia kwamba hivi karibuni kila mtu atafurahia wingi wa chakula chenye lishe.” Soma Zaburi 104:14, 15.