Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/13 uku. 4
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 5/13 uku. 4

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Juni

“Karibu kila mtu tunayezungumza naye anataka ulimwengu uwe na amani. Hata hivyo, bado kuna vita. Kwa maoni yako, kwa nini ni vigumu kupata amani ulimwenguni?” [Mruhusu ajibu.] Halafu mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti hayo, na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata. Ikiwa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 halipatikani, tumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la karibuni zaidi linalopatikana kutanikoni na pendekezo la jinsi ya kulitoa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme iliyo na pendekezo hilo.

Zingatia: Pendekezo hili linapaswa kutumiwa katika onyesho litakalofanywa kwenye mkutano wa utumishi wa shambani Juni 1.

Mnara wa Mlinzi 1 Juni 1

“Tunawatembelea watu kwenye eneo hili kwa muda mfupi ili kuzungumzia tatizo linalowapata watu wengi. Watu wengi wamewahi kubaguliwa wakati mmoja au mwingine. Je, unafikiri kuna mahali ulimwenguni ambapo hakuna ubaguzi? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Mungu anavyowaona watu. [Soma Matendo 10:34.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu atakavyokomesha ubaguzi milele.”

Amkeni! Juni

“Tungependa kujua maoni yako kuhusu jambo fulani. Ni kawaida kwa mtu kutamani maisha mazuri. Je, unafikiri tunaweza kupata maisha mazuri kwa kununua vitu vingi zaidi vya kimwili? [Mruhusu ajibu.] Ona maneno haya ya Yesu yenye maana sana. [Soma Luka 12:15.] Gazeti hili linatoa maoni yenye usawaziko kuhusu vitu vya kimwili na mapendekezo yanayofaa ya jinsi ya kudhibiti matumizi yetu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki