Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 27
JUMA LINALOANZA JUNI 27
Wimbo 123 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 5 ¶17-22 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Zaburi 52-59 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Matangazo. “Inafaa Kuripoti Muda Gani?” Hotuba itolewe na mzee. Baada ya hotuba, tumia pendekezo kwenye ukurasa wa 8 kuonyesha jinsi ya kuanzisha funzo katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Julai. Watie wote moyo washiriki katika utumishi huo.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Julai. Mazungumzo. Tumia dakika moja au mbili kupitia baadhi ya habari zilizomo katika magazeti ya karibuni. Kisha chagua makala mbili au tatu na uwaombe wasikilizaji wataje maswali na maandiko yanayoweza kutumiwa wakati magazeti hayo yanapotolewa. Panga maonyesho ya jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 15: Uwe Mwenye Busara Unapohubiri. Mazungumzo yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 197-199. Panga onyesho kumhusu mhubiri anayejibu kipingamizi cha kawaida bila busara, kisha onyesho lingine linaloonyesha akijibu kipingamizi hichohicho kwa busara.
Wimbo 92 na Sala