Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Septemba
“Watu wa mataifa na dini mbalimbali husali kila siku. Unafikiri Mungu husikiliza na kujibu sala zote?” Mruhusu ajibu, kisha umpe nakala ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mtolee magazeti, na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
Onyesha ukurasa wa juu wa gazeti na useme: “Ungejibuje swali hili? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inasema kuhusu jambo hilo. [Soma 1 Yohana 5:19.] Kulingana na andiko hili, “yule mwovu,” au Ibilisi, anautawala ulimwengu. Lakini hilo linatokeza maswali fulani. Ibilisi alitoka wapi? Je, ni mtu halisi? Mungu atamruhusu atawale kwa muda gani? Gazeti hili linaonyesha kile ambacho Biblia inasema.”
Amkeni! Septemba
“Watu wengi leo wana mikazo mingi kwa sababu ya matatizo ya kifedha. Unafikiri kwa nini ni vigumu sana kupata riziki? [Mruhusu ajibu.] Biblia ina mashauri yenye hekima ambayo yamewasaidia watu wengi kupangia vizuri matumizi yao ya pesa. [Soma mojawapo ya maandiko yaliyo katika ukurasa wa 8-9.] Gazeti hili linatoa madokezo yanayowafaa wale wanaohangaishwa na madeni.”