Ratiba ya Juma Linaloanza Novemba 28
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 28
Wimbo 26 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 13 ¶8-16, sanduku kwenye uku. 105 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Wimbo wa Sulemani 1-8 (Dak. 10)
Na. 1: Wimbo wa Sulemani 1:1-17 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Husema Kwamba Siku za Mwisho Zilianza Mwaka wa 1914?—rs uku. 289 ¶3–uku. 290 ¶2 (Dak. 5)
Na. 3: Tunaweza Kufanya Nini ili Tuheshimiwe na Wengine? (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Matangazo. Panga onyesho la jinsi funzo linavyoweza kuanzishwa katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Desemba, kwa kutumia pendekezo lililo katika ukurasa wa 4. Watie moyo wote washiriki utumishi Jumamosi hiyo.
Dak. 15: “Sifa Muhimu Zaidi ya Mwalimu Mzuri.” Maswali na majibu. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo upendo walioonyeshwa na mwalimu wao wa Biblia uliwasaidia kufanya maendeleo ya kiroho.
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Desemba. Mazungumzo. Tumia dakika moja au mbili kuzungumzia makala chache za magazeti ya karibuni ambazo huenda zikawavutia watu katika eneo lenu. Halafu, kwa kutumia makala za kwanza za Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza, na vilevile andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu makala za kwanza za Amkeni! na wakati ukiruhusu, makala nyingine moja kutoka kwa gazeti lolote kati ya hayo. Panga onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Wimbo 63 na Sala