Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Vilevile, pamoja na broshua hiyo au badala yake, makutaniko yaweza kuamua kutoa yoyote kati ya broshua zilizokuwa toleo la Agosti 2011. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu au Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kinaweza kutolewa. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia gazeti la zamani au broshua yoyote inayomfaa. Februari: Wahubiri wanaweza kutoa kimojawapo ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, na Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
◼ Michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote ambayo inatumwa moja kwa moja kwa ofisi ya tawi inapaswa kuandikwa “International Bible Students Association” nchini Kenya na Uganda, na “Association of Jehovah’s Witnesses” nchini Tanzania.